Wednesday, 20 December 2017

vitendo vya ubakaji katika Halmashauri ya mji wa Bunda Mkoni Mara bado vinaendelea kushika kasi

vitendo vya ubakaji katika Halmashauri ya mji wa Bunda Mkoni Mara bado vinaendelea kushika kasi baada ya baba mmoja mwenye umri wa miaka 37 kuripotiwa kumbaka mwanafunzi wa darasa la pili katika kata ya nyamakokoto.
Akizungumza mtoto huyo jina tunalihifadhi amesema kuwa alikuwa akishawishiwa na baba huyo kwa kumpa hela, huku akikataa na hatimae siku moja akenda kuoga bafuni akamfanyia tendo hilo la ubakaji na kumweleza kuwa asitoe taarifa kwa wazazi wake kwani akifanya hivyo atamnyonga.
Aidha mama wa mtoto ameeleza kwamba alimuona mwanae akitembea akiwa ameachanisha miguu na kumuuliza ambapo mtoto huyo alimkimbia mama yake, hivyo alilazimika kumshawishi na kumweleza kwamba alibakwa na baba huyo.
Aidha baada ya kutoa taarifa polisi aliambiwa ampeleke mtoto hospitali kwa vipimo na kuonyesha kuwa ni kweli mtoto huyo amefanyiwa kitendo hicho.

Taarifa zilizopo ni kwamba alikamatwa na polisi mtuhumiwa huyo.

Tuesday, 19 December 2017

Mama amemficha mwanae ndani kwa sababu eti mwanae ni mgonjwa wilayani Bunda

Mama mmoja majina tunayahifadhi anaeishi katika Kata ya Nyamakokoto halmashauri ya mji wa Bunda Mkoani Mara ameripotiwa kumfanyia mwanae wa kumzaa kitendo cha unyanyasaji wa kijinsi kwa kumficha ndani huku akiwa mgonjwa hali iliyompelekea mtoto huo jina tumeliifadhi kudhoofika.
Mtoto huyo mwenye miaka 9,inaelezwa kuwa ana kg.16 tu.

Aidha afisa ustawi wa jamii halmashauri ya mji wa bunda Pius Masalu amekiri kupata taarifa za mtoto huyo na kuongeza kuwa baada ya kufuatilia ilibainika kuwa jina aliloandikishwa kupata dawa hospitalini hapo ilibadilishwa mfano alikuwa anaitwa musa baadae mama yake aliamua kubadilisha jina lake na kumwita adam.

Mwanafunzi amejikuta akiingia katika ulimwengu mpya baada ya kubakwa na Baba mdogo wake ambaye ndiye mlezi wilayani Bunda

Sasu  (si jina lake halisi) ni mwanafunzi wa Darasa la sita katika shule moja ya msingi iliyoko Wilayani Bunda mkoani Mara.
Mwanafunzi huyo alijikuta akiingia katika ulimwengu mpya baada ya kubakwa na Baba mdogo wake ambaye ndiye mlezi wa mtoto huyo tarehe 12 ya mwezi wa 12 mwaka 2016  wakati akiwa darasa la tano.
Baba mdogo alimchukua ili amlee wakati akiwa bado ni mdogo.
Kulingana na mwanafunzi huyo, Baba yake mdogo huyo mwenye wake wawili alianza kumfanyia kitendo hicho chA kinyama akiwa darasa la tano.
Kulingana na mwanafunzi huyo, mara kwa mara Baba mdogo huyo ambaye kwa wakati huo alikwa amemzidi umri kwa miaka kama 48, alimwimuita katika nyumba yake pindi walipo baki wawili nyumbani na kumlazimisha kufanya tendo hilo huku akimtishia kumuua endapo atasema kwa watu.
Baba huyo alizoea kumfanyia kitendo hicho hali ambayo iliendea kumuumiza mwanafunzi huyo na ndipo alipoamua kufanya maamuzi ya kusema kwa walimu wake wa hapo shuleni lakini walimu wao wakadhani ni kama utani kulingana na maneno ya wanafunzi huyo.
“Alikuwa akiniambia nilale chini halafu ananivua nguo na kujaribu kuingiza uume wake kwangu…lakini nilikuwa naumia .alisema mwanafunzi



Lakini siku moja walimu wa shule hiyo waliamini maneno ya wafunzi huyo baada ya kuonyesha hisia za kuumizwa na kitendo hicho ndipo nao wakaamua kumfikishia taarifa mwalimu mkuu wa shule hiyo ili watafute ufumbuzi wa suala hilo.
 “Sisi walimu tulichokifanya nikwenda kwa mkuu wetu wa shule lengo nikuona mwanafunzi wetu anasaidiwa” walisema walimu
Mwalimu mkuu alisema alichokifanya aliwaita viongozi akiwemo na mwenyekiti wa kamati ya shule ,Mwenyekiti wa kijiji,na wajumbe baadhi wa kamati ya shule ili kuwapa taarifa hiyo.
 “Mimi nilichofanya nilimuuita mwenyekiti wangu wa kamati ya shule na mwenyekiti ya kijiji pamoja na wajumbe wa kamati nikawambia wao wakaamua kwenda na mwanafunzi Hospital pamoja kituo cha polisi lakini baada ya hapo mimi sijuwi kinachoendelea” anasema mwalimu mkuu
Naye Mwenyekiti wa kijiji hicho amesema ni kweli aliitwa na mwalimu mkuu wa shule hiyo na akawapa taarifa ya suala hilo lakini walichofanya waliondoka na mtoto pamoja na mtuhumiwa ambaye ndiye Baba mdogo wa mwanafunzi huyo wakaenda Hospital kuchukuwa vipimo na jibu wakapewa kuwa mwanafunzi huyo tayari kashatolewa Bikra.
Aidha amesema baada ya hapo waliongozana hadi kituo cha polisi kilichpo ndani ya kata yao na kuwapa taarifa pamoja na majibu ya vipimo na ndipo mkuu wa upelelezi katika kituo hicho akawambia waliachie jeshi la polisi kazi liweze kufanyia kazi.
“ni kweli niliitwa na mwalimu mkuu wa shule hiyo na akatupa taarifa ya suala hilo lakini tulichofanya wtuliondoka na mtoto pamoja na mtuhumiwa ambaye ndiye Baba mdogo wa mwanafunzi huyo tukaenda Hospital kuchukuwa vipimo na jibu tukapewa kuwa mwanafunzi huyo tayari kashatolewa Bikra ”
“baada ya hapo tuliongozana hadi kituo cha polisi kilichopo ndani ya kata yetu na kuwapa taarifa pamoja na majibu ya vipimo na ndipo mkuu wa upelelezi katika kituo hicho akatwambia tuliachie jeshi la polisi kazi”
“asaivi sijuwi kinachoendelea maana hata nikiuliza sipata majibu”
Redio mazingira fm tukifika katika kituo cha polisi hicho kilichotajwa lakini majibu tuliyopewa ni kuwa hawana taarifa ya mwanafunzi huyo wala taarifa yeyote kutoka uongozi wa kijiji hicho.
“Sisi hatuna taarifa ya huyo mwanafunzi mliyemtaja na hatujapokea taarifa yeyote kutoka kijiji hicho”
Ikatubidi tumtafute mama mzazi wa mwanafunzi huyo yeye amesema kuwa mwanaye amemusimulia hali ilivyo lakini alipowashirikisha watoto wake wa kiume Kaka zake na Mwanafunzi huyo walichosema ni kwamba waache tu maana mdogo wao yupo hai.
“amemusimulia hali ilivyo lakini nilipowashirikisha watoto wangu wa kiume ambao ni Kaka zake na huyo mwanangu wakaniambia mama achana na mambo hayo maana si mdogo wetu yupo hai kwamba waache tu maana mdogo wao yupo hai”
Taarifa zilipo ni kuwa mwanafunzi huyo amesafirishwa kupelekwa kwa mama yake mzazi kwa madai ya kuwa anaenda likizo lakini taariza tulizozipata kupitia chanzo chetu cha Habari ni kuwa mwanafunzi huyo mipango iliyopo ni kutorudi Shuleni.
Hata hivyo aliyeshiriki kumsafirisha kumpeleka kwa mama yake ni Yule Baba yake mdogo ambaye ndiye anayetuhumiwa kufanya kitendo hicho cha kikatili.

BADO TUNAENDELEA KUFATILIA HADI TUHAKIKISHE SUALA HILI TUNALIKAMILISHA.    

Monday, 4 December 2017

Pesa ya mahindi ya msaada yamludisha Mstaafu ofisini kujibu wilayani Bunda



Baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya Bunda mkoani Mara limetoa siku tano kuanzia leo kwa aliyekuwa afisa kilimo ambaye kwa sasa amestaafu kuhakikisha anatoa taarifa ya kujitosheleza kuhusu uchakachuaji uliofanyika katika pesa ya mahindi ya msaada yalioyogawika ndani ya  halmashauri.

Azimio hilo limetolewa leo katika kikao cha dharura cha kujadili hoja ya mkaguzi wa ndani kutoka mkoani ambapo hoja hiyo emepelekea hadi  kuimbua mambo mengine yaliyokuwa yamejificha ndani.

Akizungumza wakati wa kufunga kikao hicho Mwenyekiti wa halmashauri Isack Mahela amesema wao kama wawakilishi wa wananchi hawawezi kukaa kimya wakati pesa za wananchi zinatumika sivyo.

Hata hivyo inaelezwa kuwa anayetuhumiwa kuhusuiana na suala hilo la pesa ya mahindi ya msaada kupotea juu juu  afisa huyo ameshasitaafu hivi karibuni.

Awali madiwani wameonekana kutolizishwa na majibu ya wakuu wa idara katika mambo ya msingi yanayohusu halmashauri jambo ambalo wamesema kwa hali hiyo wataisababishia halmashauri hati mbaya.

Saturday, 21 October 2017

Bodi ya filamu tanzania yatuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha muigizaji nguli wa filamu shamila mfikirwa.

Bodi ya Filamu Tanzania imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Muigizaji nguli Shamila Mfikirwa.
Katika Salamu zake kwa Rais ya Shirikisho la Filamu Tanzania Bw. Simon Mwakifamba, Mwenyekiti wa chama cha Waigizaji Ndugu Elia Mjata na wanafamilia wa filamu na uigizaji kwa ujumla Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bi.Joyce Fissoo amesema amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba huo.
“Kwa niaba ya Bodi nachukua fursa hii kutoa pole nyingi sana kwa familia ya marehemu kutokana na kuondokewa na mpendwa wao, pia Bodi imeguswa na msiba huo na inawaombea wanafamilia kwa Mungu kuwa na moyo wa subra katika kipindi hiki kigumu” alisema Bi.Fissoo.
Mwigizaji Shamila Mfikirwa maarufu kama ‘Shamila’ amefariki dunia katika Hospitali ya Occean Road Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Oktoba, 2017 alipokuwa akipatiwa matibabu.
Innalilah Wainna Ilayhi Rajiun.
Imetolewa na

Bodi ya Filamu Tanzania.

Wazazi watakiwa kuacha kutuma watoto wao usiku dukani

Zikiwa zimesalia wiki moja wanafunzi wa kidato cha nne nchini kote kuanza mtihani wao wa taifa wazazi na walezi wametakiwa kuwa na desturi ya kuwalea watoto wao katika maadili mema na kuacha kuwatuma kwenda kununua mahitaji mbalimbali dukani nyakati za usiku kwani kufanya hivyo ni kutoa mwanya kwa watoto hao kukutana na watu wanaoweza kukatisha ndoto zao kwa kuwapatia mimba.
Hayo yamesemwa jana na mgeni rasmi katika mahafari ya 24 katika shule ya sekondari bunda mheshimiwa diwani wa kata ya kabarimu Pastory Ncheye.
Amesema suala la mimba linatokana na wazazi kutowajengea malezi mazuri watoto wao, na kutolea mfano kuwa mzazi anapomtuma mtoto kwenda kufanya biashara usiku au kununua bidhaa usiku dukani inapelekea watoto hao kukutana na watu wanaowashawisha kushiriki nao kufanya ngono hatimae kupata mimba.
Aidha amewatahadharisha wanafunzi kuacha kujihusisha na vitendo vya ngono kwani kupata mimba ni majaliwa lakini watambue kwamba kuna gonjwa hatari la ukimwi.
Mheshimiwa ncheye katika mahafari hayo ameaidi kushirikiana na shule hiyo kurekebisha gari la shule lililoaribika kwa  muda mrefu hivyo kuitaji fedha zaidi ya shilingi milioni moja kukamilika.
Pamoja na hayo pia ncheye ameaidi kuwapelekea miche ya miti ili kuhakikisha mazingira ya shule hiyo yanaendelea kuwa mazuri na ya kupendeza, na kuwasifu kwa jitihada walizozifanya za usafi wa mazingira.
Kwa upande wake mwalim mkuu wa shule hiyo Machota Kora katika risala yake amesema kuwa wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo ya upungufu wa matundu ya vyoo, vyumba vya madarasa, pamoja na uzio katika mabweni ya wanafunzi wa kidato cha tano na sita.
Hata hivyo amewaomba wazazi na walezi kushirikiana na walimu katika kuwalea watoto kwakuwa wao wenyewe hawawezi na ndiyo maana katika shule hiyo jumla ya wanafunzi watatu waliotakiwa kuhitimu na wanzao walikatisha masomo yao kwa kupata mimba.



Afisa mifugo na uvuvi wa halmashauri ya mji wa bunda Mkoani Mara bwana Rick steven Kaduri apinga takwimu ya mifugo 770 kufa.

Siku chache baada ya kituo hiki  kuripoti habari kuhusu mifugo zaidi ya 700 kufa kwa tatizo la kukosa maji na majani kwa muda mrefu, hatimae leo mkuu wa idara ya mifugo na uvuvi wa halmashauri ya mji wa bunda Mkoani Mara bwana Rick steven Kaduri amejitokeza na kupinga ukweli wa taarifa hiyo licha ya kukiri kuwa mifugo imekufa.

Amesema kuwa ni kweli mifugo imekufa katika halmashauri ya mji wa bunda, lakini ameshangazwa na idadi iliyotajwa ya mifugo zaidi ya  700 kufa huku akisema kuwa kwa taarifa walizonazo kama halmashauri nzima ni zaidi ya mifugo 1000 imekufa kwa kukoswa maji na majani kwa muda mrefu.
Amesema taarifa kama hizo zilisikika tena guta kuwa zaidi ya ng’ombe 3000 wamekufa lakini bado wanazidi kuzifanyia uchunguzi kubaini ukweli wake.
Amesema tatizo la mifugo kufa imetokana na ukame wa muda mrefu huku akitaja kuwa wafugaji waliokuwa na ng’ombe wenge ndio waathirika wakubwa hivyo amewakumbusha wafugaji kufuga kisasa ili waweza kumudu hali ya mabadiliko ya tabia ya nchi.
Hivi karibuni mtandao huu umewatembelea wafugaji wa kijiji na kata ya rwabu kutaka kujua hali ya mifugo ambapo mwenyekiti wa kijiji hicho bwana Gelad Kuzenza,  alisema kuwa kwa makisio ya chini walikuwa na ng’ombe 1500 na lakini  kwa sasa wamebaki 700 huku akieleza kuwa  bei ya ng’ombe imeshuka hadi shilingi 15,000 huku wanunuzi wakisusia kununua mifugo hiyo wakati mwingine kutokana na hali ya ya kudhoofika zaidi.
Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha wafugaji kanda ya ziwa kwa maana ya mikoa ya  Mara, simiyu shinyanga, mwanza geita na Kagera bwana Mrida mshota amekiri kuwepo kwa tatizo la mifugo mingi kufa kwa ukame na hasa ng’ombe ambapo amesema kuwa wameshaanza mikakati ya kukabiliana na tatizo hilo kwa kuanzisha mashamba ya majani kwa ajili ya mifugo yao.
Amesema zoezi hilo sio la muda mfupi kwa kuwa watanzania wengi na hasa mikoa ya kanda ya ziwa bado wanafuga ng’ombe wa kienyeji na wana mifugo mingi.
Amewataka wafugaji kuanza kubadilika kwa kufuga kisasa ili waweze kuendana na mabadiliko ya tabia ya nchi.



Jumla ya wazee 235 katika kata ya neruma wilayani Bunda Mkoani Mara wamepatiwa vitambulisho vya msamaha wa matibabu

Jumla ya wazee 235 katika kata ya neruma wilayani Bunda Mkoani Mara  wamepatiwa vitambulisho vya msamaha wa matibabu lengo ikiwa ni kuhakikisha wazee wanatambuliwa na kupewa fursa ya kushiriki katika mambo yanayohusu maisha yao ya kila siku.

Akisoma taarifa ya utoaji wa huduma za afya na stawi wa jamii Kwa mgeni Rasmi Kaimu Afisa Ustawi wa Jamii wilaya ya bunda Liberatus Kazana katika maadhimisho ya siku ya wazee Duniani yaliyofanyika Katika kijiji cha Neruma kata ya neruma Oktoba 20 amesema Halmashauri ya wilaya ya Bunda inajumla ya wazee 9,994 waliona miaka 60 na kuendelea.

Kazana Amesema kunachangamoto mbalimbali katika uendeshaji wa huduma za afya na hasa katika kuwahudumia wazee huku gharama za uendeshaji wa huduma za msamaha zimekuwa kubwa katika vituo vya kutolea huduma za afya hiyo ikitokana na idadi kubwa ya wagonjwa wanaohitaji msamaha kama vile akina mama wajawazito,watoto chini ya miaka mitano,walemavu na wazee.


Kwa upande mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ambaye ni Katibu Tawala wa wilaya ya Bunda Masalu Kisasira amesema wao kama serikali wanatambua changamoto hizo hivyo ameahidi kuzifanyia kazi huku akiwasihi wazee kuwa kioo kizuri kwa watoto wao kwa kuwaonya na kuwashauri ili kuwawezesha watoto wao kuwa na misingi bora ya maisha.

Sunday, 17 September 2017

Baa, Migahawa na Vilabu vya Pombe Vyafungwa kwa Ugonjwa wa Kipindupindu

Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mh. Reuben Mfune ameagiza bar zote, migahawa, vilabu vya pombe na grocery kufungwa kwa siku zisizojulikana kutokana na ugonjwa wa kipindupindu kuzidi kusambaa wilayani humo.

Mkuu wa wilaya ametoa taarifa hiyo kupitia Afisa habari wa wilaya hiyo Daudi Nyingo na kuwataka wananchi kuwa makini na matumizi ya maji ya mito na mifereji kwani yameathiriwa na vijidudu vya kipindupindu.

"Wananchi wote wa wilaya ya Mbarali mnatangaziwa kuwa hali ya ugonjwa wa Kipindupindu bado ni mbaya sana wilaya hapa, hivyo basi biashara zote za migahawa, vyakula vyote vinavyotembezwa, minada, vilabu vya pombe, bar, grocery zote, pamoja na mikusanyiko yote inayohusiana na sherehe, vyote vimefungwa hadi hapo mtakapotangaziwa tena"

Mkuu wa Wilaya ya Mbarali amesema kuwa mtu yoyote ambaye atakiuka maagizo hayo atachukuliwa hatua kali za kisheria

"Aidha mashine zote zitakazobainika kusaga vimea au unga wa pombe za kienyeji hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao Vilevile mnakumbushwa kwamba, maji yote ya mito pamoja na mifereji yameathiriwa na vijidudu vya Kipindupindu, hivyo basi wananchi wote mnaagizwa kuchemsha maji au kutumia vidonge vya 'water guard' pamoja na kufanya matumizi sahihi ya vyoo" alisema Mfune

Hadi kufia Septemba 15, 2017 jumla ya wagonjwa 628 wamepatikana huku jumla ya watu nane wamefariki kutokana na ugonjwa wa Kipindupindu wilayani Mbarali jijini Mbeya.

Mabasi yakamatwa usiku wa manane kwa mwendokasi

Mabasi saba ya abiria yamekamatwa  na kutozwa faini kwa kosa la mwendokasi na kutofuata sheria za usalama barabarani huku wakihatarisha maisha ya abiria.

Kamatakamata hiyo  ambayo imesimamiwa na Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani   Fotunatus  Muslim akiwa na timu ya viongozi na askari  mkoa wa Morogoro imefanyika usiku wa kuamkia leo.

Zoezi la ukamataji mabasi hayo limefanyika eneo la Dumila Wilaya ya Kilosa mkoani hapa, zoezi lilichukua takribani masaa mawili ambapo mabasi hayo yamezuiwa kuondoka mpaka asubuhi huku yakitozwa faini.

Kamanda Muslim amesema jeshi hilo halitakubali kuona maisha ya watanzania yakipotea  kutokana na uzembe wa baadhi ya madereva.

Amesema  kikosi hicho cha usalama barabarani kimeahidi kupambana na madereva wa mabasi ya abiria hasa nyakati za usiku kwani ndio wamekuwa wakiendesha kwa mwendokasi huku wakidai  serikali muda huo inakuwa imelala.

Mabasi ya abiria zaidi ya saba yanayofanya safari kati ya mkoa wa Mara (Musoma) Dar es salaam, na Mwanza- Dar es salaam yamekaguliwa na kutozwa faini.

Muslim amesema  madereva wengi wamekuwa wakifuata sheria za barabarani nyakati za mchana kwa kuhofia kukamatwa kutokana na tochi zilizopo na inapofika nyakati za usiku madereva hao wamekuwa wakitumia mwanya wa kuendesha kwa mwendo kasi.

 Akizungumzia dhamira ya Polisi  Muslim amesema ni kuwalinda raia na mali zao na kuwataka askari wa usalama barabarani kuacha kufanya kazi kwa mazoea.

Amesema doria ni endelevu na sasa itakuwa kwa nchi nzima kwa usiku na mchana huku akiwataka madereva hao kuacha kudanganyika kwa madai kuwa tochi usiku hazifanyi kazi usiku na kwamba tochi sasa zitakamata mpaka usiku.

"Nimekuja na slogani ya Kamata hii ni kwa wale madereva wasiotii na kufuata sheria na tutapambana nao kila wakati na nyakati zote na hiyo itasaidia abiria kusafiri salama na matumizi ya barabarani kuwa bora," amesema kamanda Muslim

Mmoja wa abiria aliyejitambulisha kwa jina la Leon Mwete aliyekuwa katika moja ya basi yaliyokamatwa eneo hilo la Dumila amesema zoezi hilo ni zuri na linafaa kuendelea.

Amesema hii itapunguza ajali za barabarani na kwamba kwa sasa uendeshaji wa madereva wengi ni mzuri ukilinganisha na zamani.

Naye kamanda wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Morogoro Boniface Mbao ameeleza kuwa yeye akiwa msimamizi mkuu ataendelea kusimamia na kufanya oparesheni za usiku na mchana kama maelekezo yaliyotolewa.

Friday, 15 September 2017

Wanafunzi wa shule za msingi kupigwa marufuku kuzukuka mtaani kuomba msaada wa kufanikisha mahafali



Tabia ya baadhi ya wanafunzi wa kike wa shule mbali mbali za msingi na sekondari wilayani bunda,mkoani mara,ya kuzunguka mitaani na kuwaomba wananchi wawachangie fedha  kwa ajili ya kufanikisha mahafali yao kumaliza elimu ya msingi na sekondari, imekuwa kero kwa baadhi ya wazazi na kuwaomba walimu wakuu wa shule hizo kukomesha tabia hiyo.

Hayo yamesemwa na baadhi ya wazazi walipozungumza na redio mazingira fm, na kuwaomba walimu wakuu wa shule hizo kuwaita wazazi wa wanafunzi wanaohitimu katika shule hizo ili kutafuta njia nzuri  ya kufanikisha mahafali hayo ili kuwaepusha watoto wa kike kukumbwa na vitendo vya ubakaji kutoka kwa watu wenye nia mbaya.

Baadhi ya wanafunzi wa kike ambao wamezungumza na na redio mazingira fm,wamekiri kupata majaribu mengi toka kwa baadhi ya watu wanaowafikia kwa ajili ya kuwaomba kuwachangia fedha kwa ajili ya mahafali yao,badala yake watu hao huwashawishi kufanya nao mapenzi na kuwaahidi kuwapatia fedha nyingi endapo watawakubalia tendo hilo.

Wakati serikali ikipambana vikali na kukemea baadhi ya watu wanaowarubuni wanafunzi wa kike nakuwapatia mimba,baadhi ya watu wanaoendekeza tamaa zao za mwili bado wanaendelea na tabia hiyo na kujikuta wana waharibia masomo na kukatiza ndoto za maisha yao ya baadae.


Thursday, 14 September 2017

Serikali Yaunda Kikosi Maalumu Kudhibiti Mashambilizi Ya Risasi Nchini

Wiki moja baada ya kujeruhiwa kwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu Serikali imeunda kikosi kazi kushughulikia uvunjifu wa amani nchini.

Kikosi hicho kinachoshirikisha vyombo vyote vya ulinzi na usalama pia kinashughulika na kukusanya silaha za kivita ambazo zimekuwa zikitumika.

Lissu alijeruhiwa kwa risasi Alhamisi Septemba 7 nyumbani kwake Area D mjini Dodoma na sasa anaendelea na matibabu jijini Nairobi, Kenya.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi amesema hayo bungeni leo Alhamisi akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Chambani (CUF), Yusuf Salim Hussein.

Mbunge huyo amesema hana wasiwasi na uimara, uwezo na weledi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika kusimamia majukumu yake ndiyo maana nje ya mipaka ya nchi ni salama lakini ana wasi wasi kuhusiana na hali ya usalama nchini.

“Lakini ndani ya nchi yetu hali si salama na mifano miwili ya juzi ya mbunge (Lissu) na Meja Jenerali mstaafu Vincent Mritaba inadhihirisha kwamba ndani ya nchi yetu tuna matatizo, je ni kwa nini Jeshi la Wananchi lisishiriki kikamilifu kuondosha matumizi ya silaha na mauaji ya raia wasio na hatia ndani ya nchi yetu?” alihoji mbunge huyo.

Amesema anavyoona yeye silaha za kivita zinamilikiwa na JWTZ na matumizi yake yanatakiwa yawe ya chombo hicho.

Mbunge huyo alihoji ni kwa nini wasitumike askari maalumu kuhakikisha silaha za kivita zinazotumika vibaya kuua raia zinakamatwa.

Waziri Mwinyi akijibu swali hilo amesema ni dhahiri kwamba kazi ya JWTZ ni ulinzi wa mipaka lakini pale linapohitajika au kuombwa kusaidia mamlaka zingine za kiraia au vyombo vingine vya ulinzi na usalama huwa tayari kufanya hivyo.

“Tunavyozungumza ni kwamba, mamlaka hizo ambazo ni vyombo vingine vya ulinzi na usalama vikihitaji msaada wa jeshi mara zote tunakuwa tayari kutoa msaada huo, kwa hali ilivyo sasa imeundwa task force (kikosi kazi) inayojumuisha vyombo vyote vya ulinzi na usalama ili kulifanyia kazi tatizo hili la uvunjivu wa amani ndani ya nchi,” amesema.

Amesema hana shaka na kazi hiyo imeanza, hivyo kuwahakikishia wananchi kuwa jukumu hilo litafanywa vyema ili hali ya usalama iwepo ndani ya nchi.

Dk Mwinyi amesema ni kweli silaha za kivita zinadhibitiwa na JWTZ na kwa kutumia kikosi kazi hicho, watakusanya silaha hizo kutoka kwa raia au watu wengine wote ambao wanamiliki silaha hizo ambazo kwa kawaida, utaratibu na kisheria hawapaswi kuwa nazo.

Amesema zitakapopatikana silaha hizo zitarudishwa katika mamlaka zinazohusika.

Katika swali la msingi, Mbunge wa Mkoani (CUF), Twahir Awesu Mohamed alihoji Serikali imejipangaje kuimarisha amani nchini.

Waziri Mwinyi amesema JWTZ imejipanga kikamilifu kuhakikisha mipaka ya nchi inalindwa muda wote dhidi ya adui yeyote atakayejitokeza kuivamia.

“Jeshi letu kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama, limeimarisha ulinzi katika maeneo ya mipaka yenye wakimbizi ,” amesema.

Amesema hatua hiyo imesaidia kuzuia na kukabiliana na vitendo vya kihalifu vinavyowezwa kusababishwa na wakimbizi katika mipaka na katika makambi.

Spika Job Ndugai Amtolea UVIVU Godbless Lema

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai, amejibu tuhuma za mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema, na kumtaka asipotoshe wananchi, bali apeleke malalamiko yake kwenye kamati.

Spika Ndugai ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akiendesha bunge, na kusema kwamba bunge lina utaratibu wake kwenye kila jambo linalohusika bungeni hapo.

"Lema asipotoshe wananchi aende hadharani kwenye kamati kuzungumzia hayo, bunge haliwezi kusimama kwa shambulio la Lissu bali kanuni zinasema mbunge akifariki bunge linasimama kwa siku moja. Na iwapo Spika akiletewa jambo la maadili linapelekwa kamati ya maadili, suala la jinai linapelekwa polisi", amesema Spika Ndugai

Pia Spika Ndugai amesema suala la Tundu Lissu kuchangiwa fedha za matibabu na wabunge wakati yeye alitibiwa nje ya nchi ni kwamba matibabu ya Tundu Lissu yameenda kinyume na utaratibu wa bunge.

"Wabunge wanaopelekwa nje (India) wanapewa rufaa kutoka hospital ya Muhimbili lakini si kama alivyopelekwa Lissu", amesema Spika Ndugai.

Pamoja na hayo Spika Ndugai amesema anamsamehe Godbless Lema na kuwataka watu kumsamehe kwani hajui alitendalo.

Hapo jana mbunge wa Arusha Godbless Lema alimlaumu Spika Ndugai kuwa anashindwa kutetea kiti chake, kwa kuzidi kuwakandamiza wabunge wa upinzani hususan suala la kupigwa risasi kwa Tundu Lissu.