Wanafunzi wa shule za msingi kupigwa marufuku kuzukuka mtaani kuomba msaada wa kufanikisha mahafali - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Friday 15 September 2017

Wanafunzi wa shule za msingi kupigwa marufuku kuzukuka mtaani kuomba msaada wa kufanikisha mahafali



Tabia ya baadhi ya wanafunzi wa kike wa shule mbali mbali za msingi na sekondari wilayani bunda,mkoani mara,ya kuzunguka mitaani na kuwaomba wananchi wawachangie fedha  kwa ajili ya kufanikisha mahafali yao kumaliza elimu ya msingi na sekondari, imekuwa kero kwa baadhi ya wazazi na kuwaomba walimu wakuu wa shule hizo kukomesha tabia hiyo.

Hayo yamesemwa na baadhi ya wazazi walipozungumza na redio mazingira fm, na kuwaomba walimu wakuu wa shule hizo kuwaita wazazi wa wanafunzi wanaohitimu katika shule hizo ili kutafuta njia nzuri  ya kufanikisha mahafali hayo ili kuwaepusha watoto wa kike kukumbwa na vitendo vya ubakaji kutoka kwa watu wenye nia mbaya.

Baadhi ya wanafunzi wa kike ambao wamezungumza na na redio mazingira fm,wamekiri kupata majaribu mengi toka kwa baadhi ya watu wanaowafikia kwa ajili ya kuwaomba kuwachangia fedha kwa ajili ya mahafali yao,badala yake watu hao huwashawishi kufanya nao mapenzi na kuwaahidi kuwapatia fedha nyingi endapo watawakubalia tendo hilo.

Wakati serikali ikipambana vikali na kukemea baadhi ya watu wanaowarubuni wanafunzi wa kike nakuwapatia mimba,baadhi ya watu wanaoendekeza tamaa zao za mwili bado wanaendelea na tabia hiyo na kujikuta wana waharibia masomo na kukatiza ndoto za maisha yao ya baadae.


No comments:

Post a Comment