vijana wa mgambo 166 wachukuliwa na Suma jkt wilayani Bunda - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Thursday 14 September 2017

vijana wa mgambo 166 wachukuliwa na Suma jkt wilayani Bunda

Mkuu wa wilaya ya Bunda Mkoani Mara mwl.Lydia Bupilipili amewapongeza wale wote waliojitokeza miaka ya nyuma kushiriki mafunzo ya mgambo, kwani wamekuwa msaada mkubwa ndani ya jamii katika utekelezaji wa majukumu ya ujenzi wa taifa.

Bulipili ametoa Pongezi hizo siku chache baada ya wanamgambo 166 kuchukuliwa na Suma jkt, kwajili ya kwenda kulinda katika makampuni  mbalimbali hapa nchini.

Aidha Bulipili amesema kuwa, vijana waendelee kujitokeza kwa wingi kushiriki mgambo kwani serikali ya wilayani Bunda imedhamilia kumaliza kero mbalimbali likiwemo suala la ajira.

Hata hivyo Bupilipili  amesema mngambo ni kitu muhimu sana na sio cha kubezwa hata mara moja hivyo vijana wasione aibu kushiriki kwa asilimia mia moja.


No comments:

Post a Comment