tabia ya kuanzisha masoko kiholela pasipo mpangilio yapigwa marufuku Bunda - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Thursday 14 September 2017

tabia ya kuanzisha masoko kiholela pasipo mpangilio yapigwa marufuku Bunda

Mkuu wa wilaya ya Bunda mwl. Lydia Bhupilipili amekemea tabia ya uwanzishwaji wa masoko kiholela pasipo mpangilio kwani hali hiyo  inapelekea kukosesha mapato ndani halmashauri na serikali kiujumla.
Bhupilipili ameyasema hayo hivi karibuni wakati akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake ambapo amekemea tabia hiyo na kuwataka wataalamu wa mipango miji kuhakikisha wanafanya kazi yao ipasavyo. 

Aidha Bhupilipili amemtaka mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa bunda Janeth Mayanja kuhakikisha ana wasimamia wahusika wote wa mipango miji ili waweze boresha na kusitisha uwanzishwaji wa masoko kila sehemu bila utaratibu hali inayopelekea uchafudhi wa mazingira katika maeneo hayo.


Katika hatua nyingine Bhupilipili amesema kuwa kwa sasa stendi mpya ya Mabasi kumekuwa na mbanano wa magari na kushauri kwamba utengenezwe utaratibu wa baadhi ya magari mfano yanayo kwenda nyamuswa yawe yanatokea Manjebe ili kupunguza msongamano uliopo kwa sasa katika stedi hiyo.

No comments:

Post a Comment