ng’ombe 7485 katika kata ya bunda stoo katika halmashauri ya mji wa bunda kuwekewa chapa - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Thursday 14 September 2017

ng’ombe 7485 katika kata ya bunda stoo katika halmashauri ya mji wa bunda kuwekewa chapa

Jumla ya ng’ombe 7485 katika kata ya bunda stoo katika halmashauri ya mji wa bunda  inatarajiwa kusajiliwa ikiwa ni sambamba na uwekaji  chapa zoezi litakalochukua siku 10 kukamilika.

Zoezi hilo la uwekaji chapa kwa mifugo limeanza tarehe saba mwazi huu katika kijiji cha butakale na linatarajiwa kukamilika tarehe 17  Mwezi wa tisa mwaka huu.
Akisoma taarifa fupi ya mifugo mbela ya mkuu wa wilaya ya bunda, mtendaji wa kata hiyo bwana  Raymond Bukombe amesema kuwa kata hiyo inajumla ya mifugo 27485 na yote inatarajiwa kusajiliwa.


Hata hivyo mkuu wa wilaya ya bunda Mwalimu Lydia Bupilipili amewapongeza wafugaji wa kata ya bunda stoo kwa kuhamasika kepeleka mifugo yao kuwekewa chapa na kusajiliwa kwa kuwa zoezi hilo ni la kitaifa na ni muhimu kwani inapunguza baadhi ya changamoto ikiwemo wizi wa mifugo

No comments:

Post a Comment