Lusato Masinde Afisa wanyamapori kutoka TAWA kanda ya ziwa ,picha na Catherine Msafiri
Kobe ni wanyama kama walivyo wanyamapori wengine na wanalindwa kisheria tuwatunze.
Na Catherine Msafiri,
Jamii imetakiwa kuendelea kuwatunza na kuwalinda kobe kwaajiri ya manufaa ya vizazi vijavyo kwani ujangili dhidi yao unahatarisha uwepo wa mnyama kobe kwa miaka ijayo.
Hayo yameelezwa na afisa wanyamapori kutoka TAWA kanda ya ziwa ndugu,Lusato Masinde alipofanya mahojiano na radio Mazingira fm kwenye kipindi cha uhifadhi na utalii.
Afisa wanyamapori TAWA kanda ya ziwa Lusato Masinde
Aidha Masinde ameeleza kuwa binadamu ndie kiumbe hatari zaidi kwa mnyama kobe kutokana na shughuli zao hasa pindi wanapochoma misitu Pia amebainisha kuwa mnyama kobe anafaida mbalimbali kiuchumi, kiikolojia na kijamii
Sauti ya Afisa wanyamapori kutoka TAWA kanda ziwa Lusato Masinde
Hata hivyo ameeleza sifa za mnyama kobe huku akibainisha kuwa kisheria watu wanaweza kuanzisha mashamba ya kufuga kobe isipokuwa tu kwa kuzingatia sheria na taratibu.
Sauti ya Afisa wanyamapori kutoka TAWA kanda ziwa Lusato Masinde
Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha nne kutoka Shule ya Sekondari Migungani wakiwa kwenye chumba cha kurushia matangazo radio Mazingira Fm
Wamesema kuwa ziara hiyo imewapanua uelewa wao kuhusu namna vyombo vya habari vinavyofanya kazi.
Na Taro Michael
Wanafunzi wa kidato cha nne kutoka Shule ya Sekondari Migungani, iliyopo wilayani Bunda, mkoani Mara, wamefanya ziara ya kielimu katika Redio Mazingira FM kwa lengo la kujifunza kwa vitendo kuhusu mawasiliano na utangazaji wa redio.
Ziara hiyo ni sehemu ya mtaala wa elimu unaolenga kuwajengea wanafunzi uelewa wa kina kupitia mafunzo ya vitendo, hasa katika masomo ya lugha, uraia, na teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA).
Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha nne kutoka Shule ya Sekondari Migungani wakiwa nje ya ofiza za radio Mazingira Fm
Wanafunzi hao takribani 20 walipata fursa ya kutembelea vitengo mbalimbali vya utangazaji, kujionea kwa macho namna vipindi vinavyoandaliwa, kurekodiwa na hatimaye kurushwa hewani. Pia walijifunza mbinu za ukusanyaji wa habari, uandishi wa taarifa na uhariri wa vipindi vya redio.
Aidha baadhi ya wanafunzi walieleza kufurahishwa na kile walichojifunza. Wamesema kuwa ziara hiyo imewapanua uelewa wao kuhusu namna vyombo vya habari vinavyofanya kazi na kuwaongezea ari ya kuchangia maendeleo kupitia fani ya mawasiliano.
Mkuu wa wilaya ya Bunda Mhe Aswege Enock Kaminyoge
Tangu kuanzishwa kwa jukwaa hili mwaka 2005 limesaidia wanawake wengi katika kuhakikisha wanazifikia ndoto zao
Na Adelinus Banenwa
Mkuu wa wilaya ya Bunda Mhe Aswege Enock Kaminyoge amezielekeza halmashauri za wilaya ya Bunda kuandaa program maalumu kwa ajili ya kutoa elimu ya mikopo kwa akina mama wajasiriamali ambao wanajiunga katika vikundi ili kupunguza changamoto za mikopo kwa akina mama hao
Dc kaminyoke ametoa maelekezo hay oleo may 8 2025 katika uzinduzi wa chemba ya wanawake wajasiriamali wilaya ya Bunda chini ya TANZANIA WOMEN CHEMBER OF COMARCE.
Sauti ya Mhe Aswege Enock KaminyogeBaadhi ya wanachama na wanufaika wa chemba TWCC
Baadhi ya wanachama na wanufaika wa chemba hiyo wamesema kuna fursa mbalimbali kwa wanawake kujiunga na umoja huo kutokana na kukutanishwa na wataalamu mbalimbali pamoja na taasisi za serikali zinazowapatia elimu ili kukabiliana na changamoto za kibiashara katika ujasiriamali wao
Aidha wametoa wito kwa wanawake wengine kutoogopa kujiunga na jukwaa hili kwa kuwa wapo walioanza pasipo kuwa na uelewa lakini hadi hivi sasa wametengeneza mtandao mkubwa wa biashara.
sauti ya wanufaika wa jukwaa la TWCCBaadhi ya wajasiriamali waliojiungq na jukwaa la TWCC wakionesha walivyoongeza thamani Bidhaa zao
Kwa upande wake mkurugenzi wa jukwaa hili la TWCC Maria Isidory amesema tangu kuanzishwa kwa jukwaa hili mwaka 2005 limesaidia wanawake wengi katika kuhakikisha wanazifikia ndoto zao katika kuwasaidia elimu ya biashara, mitaji na kuwakutanisha na wataalamu pamoja na taasisi za serikali kama vile TRA, SIDO miongoni mwa taasisi zingine
Sauti ya mkurugenzi wa jukwaa hili la TWCC Maria Isidory
Wateja wamepungua kwa kasi katika siku za hivi karibuni kutokana na watu wengi kuelekeza nguvu zao katika kununua samaki
Na Thomas Masalu
Imeelezwa kuwa katika mji wa Bunda, upatikanaji mkubwa wa samaki kwa sasa umeanza kuathiri kwa kiasi kikubwa biashara ya nyama ya ng’ombe, hali inayowatia hofu baadhi ya wafanyabiashara wa nyama hiyo.
Wafanyabiashara hao wamesema kuwa wateja wamepungua kwa kasi katika siku za hivi karibuni kutokana na watu wengi kuelekeza nguvu zao katika kununua samaki ambao wanapatikana kwa wingi sokoni.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti leo Mei 7, 2025, na redio Mazingira FM katika eneo la genge la jioni, wafanyabiashara hao wameeleza kuwa tofauti ya bei kati ya samaki na nyama ya ng’ombe imechangia kushuka kwa mzunguko wa biashara yao.
Wafanyabiashara hao wamesema kuwa licha ya changamoto hiyo, bado wana matumaini kuwa hali itabadilika pindi upatikanaji wa samaki utakapopungua.
Serikali tayari imetoa bilioni 53 kwa ajili ya ulipaji wa fidia kwa wakazi hao ili kuachia maeneo hayo yawe sehemu ya hifadhi ya taifa ya Serengeti.
Na Adelinus Banenwa
Wananchi wa Nyatwali ambao tayari wamelipwa stahiki zao kwa utaratibu wa kisheria watakiwa kuondoka.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Mara Kanal Evance Mtambi katika kilele cha maadhimisho ya siku ya urithi wa dunia na afrika yaliyofanyika wilayani Serengeti mkoani Mara leo tarehe 5 May 2025.
Kanal Mtambi amesema serikali tayari imetoa bilioni 53 kwa ajili ya ulipaji wa fidia kwa wakazi hao ili kuachia maeneo hayo yawe sehemu ya hifadhi ya taifa ya Serengeti.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria maadhimisho ya siku ya urithi duniani
Kanal Mtambi amesema eneo la Nyatwali tangu enzi za ukoloni lilionekana si sehemu salama kwa makazi ya binadamu na wakati huo lilitambulika kama guba ya speek na utaratibu wa wananchi waliokuwa eneo hilo kuhamishwa ulianza muda mrefu lakini serikali ya awamu ya sita imefanikisha jambo hilo.
Aidha mkuu wa mkoa wa Mara amesema kiasi cha malipo kilichosalia kinaendelea kulipwa kwa utaratibu uliowekwa
Ndege Makebe Karando (31) amuua kwa kumchoma visu aliyekuwa mpenzi wake ambaye ni muhudumu wa afya katika zahanati ya marambeka Zawadi John Kazi (35) kisha na yeye kujinyonga.
Na Adelinu Banenwa
Vilio na sintofahamu vimeendelea kutawala kwa wakazi wa kijiji cha Marambeka kata ya Ketare halmashauri ya wilaya ya Bunda kufuatia tukio la Ndege Makebe Karando (31) kumuua kwa kumchoma visu aliyekuwa mpenzi wake ambaye ni muhudumu wa afya katika zahanati ya marambeka Zawadi John Kazi (35) kisha na yeye kujinyonga.
Makebe Karando baba mzazi wa ndege amesema tukio hilo la kijana wake kufanya mauaji kisha na yeye kujinyonga limewaachia majonzi makubwa kutokana na wote waliopoteza maisha alikuwa akiwachukulia kama watoto wake.
Mama mzazi wa Ndege Makebe
Makebe amesema karando alikuwa na wake wawili lakini pia alikuwa na mahusiano na muhudumu huyo wa afya na tayari walishajitambulisha kwake na mara ya mwisho ilipotokea sintofahamu baina yao walimfikia na akawashauli na walimuhakikishia kuwa mgogoro umeisha hadi pale alipopata taarifa za tukio la mtoto wake Ndege kumshambulia Zawadi
Makebe anaeleza kuwa majira ya usiku alipokea taarifa za Zawadi kushambuliwa na Ndege lakini alikuwa hajamuona ndege japo taarifa za ujio wake pale kijijini alikuwa nazo kwa kuwa mtoto wake huyo anaishi maeneo ya Mugumu Serengeti ambako ana mke mwingine
Familia ya Ndege Makebe wakiwa msibani
Ameongeza kuwa wakati asubuhi kesho yake wanajiandaa kama nzengo kujikusanya ili waanze kumtafuta ndege na kumtia nguvuni kutokana na tukio alilolifanya ndipo alipopata taarifa kuwa mtoto wake huyo amekutwa shambani akiwa amejinyonga kwenye mti aina ya mkwaju na alpokwenda alishuhudia kweli Ndege amejinyonga
Makebe Karando
Ngei Mashoka rafiki wa karibu wa ndege ameiambia Mazingira fm kuwa aligundua kuwa rafiki yake amejinyonga baada ya kupigiwa simu kutoka Musoma kutoka kwa rafiki yao mwingine akidai amepokea simu kutoka kwa Ndege akidai anaenda kujiua kwa kujinyonga katika moja ya miti iliyo shambani mwake
Ngei Mashoka rafiki yake Ndege na liyegundua kuwa Ndege amejinyonga
Huku rafiki huyo akieleza kuwa maelekezo ya ndege yalikuwa endapo watamkuta ameshakufa wamtumie nauli mke wake aliyeko Mugumu aje kwenye msiba
Ngei Mashoka
Hata hivyo baadhi ya viongozi katika kijiji hicho akiwemo diwani wa kata ya Ketare Mramba Simba Nyamkinda na mwenyekiti wa kijiji Ramadhani Lukiko wamekemea tabia za vijana kujichukulia sheria mkononi huku wakitoa wito kuwa endapo kuna sintofahamu kwa watu wenye mahusiano ni vema wakapata suluhu kutoka kwa viongozi
viongozi diwani na mwenyekiti
Jeshi la polisi kupitia kwa kamanda wa polisi mkoa wa Para Pius Lutumo limethibitisha kutokea kwa matukio hayo mawili yaani kuuawa kwa Zawadi John na Ndege Makebe kujinyonga kwenye mti kwa kutumia shuka huku chanzo cha tukio hilo kikitajwa kuwa ni wivu wa kimapenzi baada ya marehemu Zawadi kukataa kuendelea kuwa na mahusiano na Ndege.
Zawadi John Kazi aliyekuwa muhudumu wa afya katika zahanati ya Marambeka inatajwa ameacha watoto wawili huku Ndege Makebe akitajwa kuacha wajane wawili na watoto watano
Katika utetezi wake mshitakiwa aliiomba mahakama imuachie huru kutokana na yeye kuwa ni mjane na ana watoto watano wanamtegemea.
Na Adelinus Banenwa
Mahakama ya wilaya ya Bunda imemuhukumu kifungo cha masharti (condition discharge) cha kutokutenda kosa lolote ndani ya miezi sita Neema Msimu John(28), Mkazi wa mtaa wa Mapinduzi kwa kosa la ukatali dhidi ya mtoto wake mwenye umri wa miaka minne kwa kumchoma moto kwenye mkono wake wa kushoto kwa kosa la kujisaidia hovyo.
Hukumu hiyoimetolewa na Hakimu mkazi Mwandamizi wa mahakama ya wilaya ya Bunda, Betron Sokanya, baada ya mshitakiwa kukiri kutenda kosa hilo ambalo ni kinyume na kifungu Cha 169A(1) na (2) cha kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2022.
Katika utetezi wake mshitakiwa aliiomba mahakama imuachie huru kutokana na yeye kuwa ni mjane na ana watoto watano wanamtegemea huku mmoja wapo akiwa ananyonya.
Neema Msimu John
Awali kabla ya hukumu kutolewa, mwendesha Mashtaka wa Jamuhuri Aristariko Msongelo ameiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa ili iwefundisho kwa jamii kuacha tabia ya ukatili dhidi ya watoto.
‘‘Naomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshitakiwa ili iwe fundisho kwa jamii kuacha tabia ya ukatili dhidi ya watoto’’. Aristariko Msongelo mwendesha mashitaka wa Jamhuri Wilaya ya Bunda.
Aidha Afisa ustawi wa jamii Wilaya ya Bunda Florence Debogo awewaasa wazazi kutotumia adhabu kali kwa watoto na badala yake watumie adhabu mbadala kama kumnyima mtoto kuangalia television na kuto kwenda kucheza ili kupunguza wimbi la ukatili kwa watoto.
Wito umetolewa kwa wananchi kuzingatia usafi wa mazingira na matumizi sahihi ya vyandarua ili kuepuka maambukizi ya malaria
Hayo yamesemwa leo na Dr Henry Lukamisa ambaye ni mratibu wa Malaria mkoa wa Mara wakati akizungumza kupitia Radio Mazingira fm ndani ya kipindi cha Asubuhi leo
Amesema hadi sasa kwa mkoa wa Mara kiwango cha ugonjwa wa malaria ni asilimia 15.
Dr Henry Lukamisa ambaye ni mratibu wa Malaria mkoa wa Mara
Dr Henry amesema ugonjwa wa malaria umeua watoto takribani 62 kwa mkoa wa Mara kwa mwaka 2024 kwa vifo vilivyorekodiwa hivyo ni vema wananchi wakachukua tahadhari
Dr Henry Lukamisa
Naye Mohamed Mlanza ambaye ni mratibu wa malaria halmashauri ya mji wa Bunda ambapo amesema kwa halmashauri hiyo wanajitahidi kutekeleza afua mbalimbali za kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa malaria ikiwa ni pamoja na kugawa vyandarua kwa mama wajawazito na kwa akina mama wenye watoto wachanga.
Mohamed Mlanza ambaye ni mratibu wa malaria
Aidha Mlanza ameongeza kuwa mbali na kutoa vyandarua pia idara hiyo inatoa elimu kwa jamii juu ya namna unavyoenezwa na kusambaa pamoja na madhara ugonjwa huo.
Mohamed Mlanza
Ikumbukwe kuwa kila tarehe 25 April kila mwaka Dunia huadhimisha siku ya malaria ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu ni ” Malaria inatokomezwa na sisi, wekeza chukua hatua, ziro malaria inaanza na mimi”
Mbali na kifungo cha miaka 30 pia mahakama imeamuru kulipa fidia ya shilingi milioni 2 kwa muhanga kwa mujibu wa sheria ya uendeshaji wa makosa ya jinai 348 (1) sura ya 20 marejeo ya mwaka 2022.
Na Adelinus Banenwa
Mahakama ya wilaya ya Bunda imemuhukumu kifungo cha miaka 30 jela na fidia ya shilingi milioni 2 Vicent Joseph Nkunguu (39) aliyekuwa mwalimu mkuu wa shule msingi masaunga wilayani Bunda kwa kosa la ubakaji na ulawiti wa mwanafunzi (16) wa darasa la sita ambaye jina lake limehifadhiwa.
Hukumu hiyo ya kesi ya jinai namba 7623 ya mwaka 2024 imetolewa leo tarehe 23 April 2025 na hakimu mkazi mwandamizi wa mahakama ya wilaya ya Bunda mhe Betron Sokanya
Akisoma hukumu hiyo Mhe Sokanya amesema mahakama imejiridhisha bila kuacha shaka kuwa mtuhumiwa Vicent Joseph Nkungu alitenda kosa hilo baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili ambapo upande wa mashtaka uliwasilisha mashahidi watano (5) na kielelezo kimoja huku upande wa utetezi ukiwasilisha mashahidi wawili (2) bila kielelezo chochote.
Mhe Sokanya amesema katika kosa la kwanza la ubakaji mahakama imemtia hatiani kutokana na mshitakiwa huyo kutenda kosa angali akijua ni kinyume na kifungu cha 130 (1) (2)( e) na kifungu cha 131 (1) cha sheria ya kanuni ya adhabu sura 16 marejeo ya mwaka 2022
Aidha katika kosa la pili la kulawiti Mhe Sokanya amesema mahakama imemkuta mshitakiwa na hatia kinyume na kifungu cha cha 154 (1) (a) cha kanuni ya adhabu sura 16 marejeo ya mwaka 2022.
Mbali na kifungo cha miaka 30 pia mahakama imeamuru mshitakiwa Vicent kulipa fidia ya shilingi milioni 2 kwa muhanga kwa mujibu wa sheria ya uendeshaji wa makosa ya jinai 348 (1) sura ya 20 marejeo ya mwaka 2022.
Awali Mwendesha mashtaka wa serikali Isiaka Ibrahim Mohamed alisema matukio hayo yalitendeka tarehe 9 March 2024 nyumbani kwa mshitakiwa huku mwendesha mashtaka akiiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa ili liwe fundisho kwake na kwa wengine wenye tabia kama zake
Katika utetezi wake mshitakiwa aliiomba mahakama impunguzie adhabu kwa sababu ni mara yake ya kwanza kukutwa na hatia pia ana mke na watoto wanaomtegemea.
Mhe hakimu Sokanya amesema rufaa ipo wazi kwa hukumu hiyo.
Picha ya pamoja washiriki wa mafunzo kwa radio jamii Tanzania yaliyotolewa na TAMWA kwa kushirikiana na TADIO jijiji Dodoma
Licha ya sensa ya watu na makazi ya 2022 kuonesha idadi ya wanawake ni wengi kuliko wanaume, katika nafasi za uongozi kwa ngazi za udiwani na ubunge bado kuna idadi ndogo zaidi ya uwakilishi.
By Edward Lucas
Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania TAMWA kwa kushirikiana na TADIO wameendesha mafunzo kwa radio za kijamii Tanzania Bara kuandaa habari na vipindi vitakavyowawezesha wanawake kushiriki kikamilifu hasa kwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi mkuu wa 2025.
Akizungumzia mafunzo hayo, Meneja Mipango na Mikakati TAMWA, Sylivia Daulinge amesema mafunzo hayo yanayodhaminiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Vyombo vya Habari Finland VIKES yamelenga elimu ya namna bora ya kuandaa vipindi vya usawa na ujumuishi wa masuala ya kijinsia kwa kuhakikisha wanawake hasa vijana na makundi maalumu yanapewa kipaumbele kuelekea uchaguzi mkuu.
Sylivia Daulinge, Meneja Mipango na Mikakati TAMWASylivia Daulinge, Meneja Mipango na Mikakati TAMWA
Kwa upande wake Mkufunzi wa mafunzo hayo kutoka Radio Tadio, Hilali Alexander Ruhundwa amesema kwa kushirikiana na TAMWA wameona wanajukumu la kufanya katika jamii kwa kuwashirikisha waandishi wa habari ili kufikisha elimu kwa jamii kuwafanya wanawake washiriki kikamilifu katika uchaguzi ujao
Hilali Alexander Ruhundwa, Mkufunzi wa mafunzo kutoka Radio Tadio akieleza kuhusu malengo ya mafunzo kwa radio za jamii kuelekea uchaguzi wa 2025Sauti ya Hilali Alexander Ruhundwa
Kwa takwimu za uchaguzi mkuu uliopita wa mwaka 2020, madiwani wanawake waliochaguliwa kwenye kata ni 260 kati ya 3,953 ambao ni sawa na asilimia 6.58 na kwa upande wa ubunge kati ya majimbo 264 wabunge wanawake waliochaguliwa kwenye majimbo ni 26 tu sawa na asilimia 9.85
Ni aliyekuwa mkurugenzi mtendaji wa TANESCO aliyefariki kwa ajali ya gari eneo la nyatwali Bunda
Na Adelinus Banenwa
Shughuli ya mazishi ya aliyekuwa mkurugenzi wa TANESCO Boniface Gissima Nyamo-hanga inaendelea nyumbani kwake Mtaa wa Migungani kata ya Bunda stoo Bunda mjini mkoani Mara .
Ibada ya Mazishi ikiongozwa na Askofu Mwita Maguge wa kanisa la kiinjiri la kirutheli Tanzania KKKT dayosisi mkoani Mara.
Katika ujumbe wake kwenye ibada hiyo askofu Mguge amesema hakuna mtu anayeweza kukikimbia kifo hata kama una ulinzi wa namna gani kifo kitakufuata.
Viongozi mbalimbali wamefika katika shughuli hizo zinaongozwa na Naibu waziri mkuu na waziri wa Nishati Mhe Dotto Biteko ambapo pia amesema tanesco na na taifa kwa ujumla limempoteza mtu muhimu sana ambaye mara zote alikuwa si mtu wa kulalamika bali akiona tatizo basi anatoa na njia ya kutatua tatizo hilo.
Akisoma wasifu wa marehemu Gissima Nyamo-hanga, Irene Gowele afisa mawasiliano TANESCO amesema Mhandisi Gissima alizaliwa tarehe 10 Sept 1969 mkoani Mara huku akishika nyadhifa mbalimbali za uongozi ikiwemo mkurugenzi mkuu wa REA kati ya mwaka 2016 hadi 2019, wakala wa ujenzi Tanzania. TBA na baadae kuwa Mkurugenzi mtendaji wa TANESCO Tanzania ambapo hadi umauti alikuwa akitumika katika nafasi hiyo
Mhandisi Boniface Gissima Nyamo-hanga ameacha wajane wawili na watoto 15.
Ikumbukwe Mhandisi Nyamo-hanga alifariki dunia April 13, 2025 katika ajali ya gari eneo la Nyatwali Bunda