Chama cha wafugaji chatoa msimamo wake uwekezaji bandari - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Thursday 10 August 2023

Chama cha wafugaji chatoa msimamo wake uwekezaji bandari

 

Mrida Mshota mwenyekiti wa wafugaji Tanzania, Picha na Adelinus Banenwa

Wafugaji wanaona yapo manufaa makubwa kwenye uwekezaji wa bandari hivyo wanaunga mkono jitihada zote za serikali katika uwekezaji huo.

Na Adelinus Banenwa

Chama cha wafugaji Tanzania kupitia kwa mwenyekiti wake kimesema kinaunga mkono mkataba wa mashirikiano ya serikali na kampuni ya DP World ya Dubai unaohusu uwekezaji katika bandari

Akizungumza msimamo huo wa chama cha wafugaji Tanzania mwenyekiti Mrida Mshota amesema wao kama wafugaji wanaona yapo manufaa makubwa kwenye uwekezaji wa bandari hivyo wanaunga mkono jitihada zote za serikali katika uwekezaji huo.

Sauti Mrida Mshota mwenyekiti wa wafugaji Tanzania

Wakati mwenyekiti wa wafugaji taifa akitoa msimamo huo mahakama kuu kanda ya mbeya leo augost 10  imetupilia mbali shauri la kesi ya kupinga uwekezaji wa bandari iliyofunguliwa mahakamani hapo.

No comments:

Post a Comment