Mwili mwingine wapatikana waliozama ziwa Victori vifo vyafika 3 - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Tuesday 1 August 2023

Mwili mwingine wapatikana waliozama ziwa Victori vifo vyafika 3

wakazi wa vijiji ndani ya kata ya Igundu wakisubili kujua hatma ya ndugu zao wanahofiwa kufa maji, Picha na Adelinus Banenwa

Mwili mwingine wa muumini wa kanisa la KTMK umepatikana jioni hii na kufanya jumla ya waliopatikana kufika wawili huku vifo vikifikia vitatu kati ya watu 28 waliokuwa kwenye mitubwi iliyozama.

Na Adelinus Banenwa

Katika zoezi la utafutaji wa miili ya watu wanaohofiwa kufa maji likiendelea mwili wa mtoto mwingine umepatikana majira ya jioni na kufikisha idadi ya waliothibitika kupoteza maisha kufikia watatu 3  

Mwili uliopatikana jioni hii ni wa Rahel Pius (12) mkazi wa Buwela kijiji cha Igundu ambaye ni mwanafunzi wa darasa la 5 shule ya msingi Bulomba ambaye mwili wake umekabidhiwa kwa familia na mazishi yatafanyika kesho kwa mujibu wa taarifa ya familia.

Waliopatikana leo ni Pendo Charles (13) mkazi wa Sunsi mwanafunzi wa darasa la 7 shule ya Msingi Bulomba ambaye tayari mwili wake umekabidhiwa kwa familia kwa ajili ya kuendelea na shughuli za mazishi na Rahel Pius (12) mkazi wa Buwela kijiji cha Igundu ambaye ni mwanafunzi wa darasa la 5 shule ya msingi Bulomba ambaye mwili wake umekabidhiwa kwa familia na mazishi yatafanyika kesho kwa mujibu wa taarifa ya familia.

Mwili wa Pendo ulipatikana majira ya saa saba mchana huku Rahel akipatika majira ya saa 11 jioni

Indelea kufuatilia  taarifa zetu kupata …..updates… ya zoezi linavyokwenda ………….

No comments:

Post a Comment