Ujenzi wa Shule Shikizi Kihumbu wa milioni 348.5 utakamilika 30 July 2023, Mbunge Getere autembelea - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Tuesday 18 July 2023

Ujenzi wa Shule Shikizi Kihumbu wa milioni 348.5 utakamilika 30 July 2023, Mbunge Getere autembelea

 

Mbunge Mwita Getere akiwa katika moja ya vyumba vya madarasa ya shule shikizi Kihumbu akiangalia utekelezaji

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa Shule hiyo, Gatida Maregesi ambaye ni mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kihumbu amesema mradi huo uliopo eneo kitongoji cha Sabasita uko chini ya shule ya Msingi Kihumbu kata ya Hunyari jimbo la Bunda ambao ulipokea kiasi cha shilingi milioni 348.5 kupitia mradi wa 'BOOST'

Amesema fedha ya mradi huo iliingia tarehe 21 April 2023 ambapo utekelezaji wa mradi huo kupitia 'Force Account' ulianza tarehe 19 Mei 2023 na ulitarajiwa kukamilika tarehe 30 June 2023 lakini baadaye muda uliongezwa hadi tarehe 30 July 2023 ndipo unatarajiwa kukamilika.







Gatida amesema vyumba tisa (9) vya madarasa vimeshaezekwa na sasa wako katika hatua ya 'kuskimu', vyoo matundu 8 vimekamilika na kuezekwa, jengo la utawala linakamilika kupigwa 'lipu' na hivyo kufikia tarehe 30 July 2023 mradi utakuwa umekamilika na kukabidhiwa.







No comments:

Post a Comment