Mazingira fm waipa tano TADIO kwa mafunzo - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Saturday 8 July 2023

Mazingira fm waipa tano TADIO kwa mafunzo

Muhariri wa Radiotadio Hilali Luhundwa akiwa anatoa mafunzo kwa wafanyakazi wa Radio Maingira Fm, Picha na Edward Lucas

Mtandao wa radio za kijamii Tanzania TADIO waendelea kuwajengea uwezo waandishi wa habari kutoka redio za kijamii namna ya kutumia mitandao ili iwe fulsa kwao,

Na Catherine Msafiri na Avelina Sulusi

Wito umetolewa kwa viongozi wa redio za kijamii kusimamia waandishi ili mafunzo ya matumizi ya redio mtandao  wanayoyapata yasaidie kuleta mabadiriko katika redio zao

Wito huo umetolewa Julay 7,2023 na Hilali Alexerder Luhundwa  ambaye ni muhariri wa Radiotadio iliyoko chini ya Mtandao wa radio za kijamii Tanzania TADIO  wakati akizungumza na Mazingira Fm alipofika kituoni hapo kwaajiri ya kutoa mafunzo ya namna ya kuchapisha habari katika mtandao.

lengo kuu likiwa ni kuziunganisha redio za kijamii zitumie jukwaa hilo kubadirishana habari.

Hilali  amebainisha kuwa kutokana na mafunzo wanayotoa wanatarajia kuona radio zinabadirika na kuwa kwenye mitandao ya kijamii lakini pia waandishi wanatumia mwanya huo kama fulsa kwao hasa ukizingati teknolojia inabadirika kila siku hivyo waandishi na redio zinalazimika kubadirika kulingana na teknolojia.

Mafunzo yakiendelea kwa waandishi wa Mazingira Fm
Hilali Alexerder Luhundwa  muhariri wa Radiotadio

Aidha amebainisha kuwa TADIO  kama Mtandao wa radio za kijamii Tanzania wamelazimika kuanzisha jukwaa la redio mtandao lengo kuu likiwa ni kuziunganisha redio za kijamii zitumie jukwaa hilo kubadirishana habari.

Hilali Alexerder Luhundwa  muhariri wa Radiotadio

Kwa upande wao waandishi wa habari wa kituo cha radio Mazingira Fm wameishukuru tadio kwa mafunzo waliyoyapata na  kutokana na mafunzo hayo wamejua namna ya kuchapisha habari kwenye mtandao pia kutumia mitandao ya kijamii kama fulsa  .

Aidha wameiomba  TADIO  kuendelea kutoa mafunzo haya ili yaendelee kuwajenga na kuendana na kasi ya mabadiriko ya technolojia duniani

Wandishi kutoka Mazingira Fm

No comments:

Post a Comment