Monday, 28 May 2018
Sunday, 27 May 2018
Friday, 25 May 2018
WAKULIMA wa zao la pamba wilayani Bunda mkoani Mara hadi sasa wamegoma kuuza pamba zao kwa vyama vya msingi
WAKULIMA wa zao la pamba wilayani Bunda mkoani Mara hadi sasa wamegoma kuuza pamba zao kwa vyama vya msingi kwa kile wanachodai kuwa hawana imani na vyama hivyo ambavyo viliwadhuluma hapo awali.
Kitendo hicho kimewafanya baadhi ya mawakala wa makampuni waliojitayarisha katika vituo mbalimbali kushirikiana na vyama vya msingi kufunga virago vyao baada ya kukaa vituoni bila kuwaona wauzaji.
Hali hii imetokea katika vijiji vya Kunzugu, Bukole, Miale,Nyamatoke na baadhi ya maeneo huku wakiishutumu vikali serikali kuwa imechukua hatua za haraka kukabidhi majukumu hayo kwa vyama vya msingi kabla ya kufanya utafiti wa kina.
Aidha wakulima hao wamedai hawatauza pamba zao huku baadhi yao wakisema kuwa hali hiyo ikiendelea watahaahirisha kulima zao hilo katika msimu ujao na kwamba serikali inachangia kuandaa kifo cha zao hilo maarufu ya biashara.
Shija Maduhu(48) mkazi wa Kijiji cha Bukole akizungumza na mwandishi wa habari hizi alidai wakulima hawako tayari kuuza zao hilo kwa mfumo wa sasa hadi serikali ione umuhimu wa kufanya marekebisho.
“Tumetishwa na hali hii, kwanza vyama hivi vya msingi vya wakulima vilitunyanyasa sana katika kipindi kilichopita, fedha zetu zililiwa kwa mfumo huu………” alisema Maduhu.
“ we ni mwandishi wa habari, unajua wazi kwamba kutokana na mfumo huu wa kuuza zao lako na fedha kuchukuliwa baadaye wakulima walidhulumiwa mpaka mali ya vyama hivi vilitaifishwa kutokana na madeni, leo bila kupitia mchakato imara mfumo ule unarudishwa, kwa kweli serikali itusamehe katika hili.
“Mara Co-operative Union (MCU) kiko wapi, nani alikiua, tuna jineri hapa ya Ushashi bado iko chini ya mfilisi vyote vilivyouawa na mfumo huu wa vyama vya msingi…. Ni vyema serikali ingekaa nasi tujadiliane tufanye nini” alisisitiza.
Aidha alidai kitendo cha agizo la serikali la kutaka kila mkulima wa pamba afungue akaunti ili fedha za mauzo yake yatumwe kwenye akaunti yake inalenga fedha hizo kukatwa bila ridhaa za wakulima.
Wamedai walilima kwa furaha wakitegemea kupata fedha lakini matumaini yao yanaendelea kufifia huku wakikabiliwa na hali ngumu ya uchumi wakati ambapo wanafanya matayarisha ya kuwapeleka shule watoto katika muhula wa pili unaoanza mwezi Julai.
Hivi karibuni akifungua msimu wa mauzo ya pamba mkoani Mara katika Kijiji cha Bukole wilayani Bunda , mkuu wa mkoa wa Mara aliagiza kila mkulima wa pamba kuhakikisha anafungua akaunti benki ili atakapouza pamba yake fedha zake ziwekwe kwenye akaunti yake na si vinginevyo.
Pia Malima alitoa tahadhari kuwa mkulima yeyote ambaye atauza pamba zake holela au kwa kampuni yoyote bila kupitia vyama vya msingi atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Mkuu wa wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili na watendaji wake wilayani Bunda inawasisitizia wakulima wa Bunda kuuza pamba zao katika vyama vya ushirika ingawa toka msimu wa manunuzi ufunguliwe Mei Mosi mwaka huu bado wakulima wengi hawajauza pamba zao.
Thursday, 24 May 2018
Zahanati ya kijiji cha kurusanga iliyopo kata ya Salama wilaya ya Bunda Mkoani Mara kimepokea msaada wa Darubini kutoka kwa Diwani wa Kata ya Ketare
Zahanati ya
kijiji cha kurusanga iliyopo kata
ya Salama wilaya ya Bunda Mkoani Mara
imepokea msaada wa Darubini kutoka kwa Diwani wa Kata ya
Ketare mh.Mramba Simba Nyamkinda
itakayotumika kupima magonjwa
mbalimbali na kuboresha huduma katika zahanati
hiyo.
Darubini
hiyo yenye thamani ya shiliingi milioni
moja inayotumia nishati ya umeme na jua imetolewa jana jumamosi na mh.Mramba Simba
Nyamkinda ambae ni diwani wa kata
ya Ketare baada ya kuona ukosefu wa kifaa hicho katika zahanati hiyo.
Akizungumza wakati
wa kupokea kifaa hicho Daktari msimamizi wa Zahanati hiyo Sajadi
Hassani amemshukuru mheshimiwa Mramba
ambapo amesema awali walikuwa wakitoa huduma kwa kukisia ugonjwa lakini sasa darubini hiyo itawasaidia kubaini
magojwa na kutoa huduma kwa uhakika.
Pia Mramba
amemtaka daktari wa kituo hicho kutunza vizuri kifaa hicho ili kiwasaidie wananchi kupata huduma za vipimo ambapo amewaomba wasikipoteze kama walivyo poteza Darubini
aliyoitoa hapo awali.
Wakati huo
huo mh.Mramba ametoa pawa miksa katika kanisa la EAGT la kurusanga na kuahidi kutoa mifuko kumi ya
sementi ili kuendeleza ujenzi wa kanisa hilo.
Bulaya Aitupia Lawama Serikali....Adai Imesababisha TANESCO Ifiilisike
Mbunge
Bunda Mjini (Chadema), Ester Bulaya amesema Serikali ya Awamu ya Tano
tangu ilipoingia madarakani Novemba 5, 2015 imelifanya Shirika la Umeme
Tanzania (Tanesco) kushindwa kujiendesha kwa faida, kutaka ligawanywe.
Bulaya
ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Mei 24, 2018 bungeni mjini Dodoma katika
mjadala wa bajeti ya Wizara ya Nishati mwaka 2018/19.
Amesema
kwa muda mrefu ripoti mbalimbali za kamati za Bunge, ikiwamo ya
mashirika ya umma, zinaeleza namna Tanesco inavyojiendesha kwa hasara.
Amesema
kabla ya Serikali hiyo haijaingia madarakani, Tanesco ilikuwa ikipata
hasara ya Sh124 bilioni lakini baada ya kuingia madarakani Tanesco
inapata hasara ya Sh346 bilioni inayotokana na upugufu wa maji na
gharama za uendeshaji.
“Tanesco
ina madeni ambayo yamepanda kwa asilimia 23. Kabla Serikali hii
haijaingia madarakani, Tanesco walikuwa na madeni ya Sh738 bilioni
lakini baada ya kuingia yamefikia Sh958 bilioni na haya si maneno ya
Bulaya. Ukiangalia ripoti ya CAG, inasema madeni hayana uhusiano kati ya
Tanesco na mali, kwa maana nyingine Tanesco imefirisika,” amesema
Bulaya.
Amesema
wakati madeni haya yanatokea, kulikuwa na ushauri na mikakati
mbalimbali ya kuligawanya shirika hilo ili kutenganisha usambazaji na
uzalishaji.
“Leo
hii tusingekuwa tunazungumza umeme wa vibaba wakati tunataka Tanzania
ya viwanda. Wakati haya yanafanyika, Tanesco inashindwa kukusanya madeni
makubwa, Tanesco inaidai Hospitali ya Tumaini Dola milioni 9.4 za
marekani sawa na Sh18 bilioni na ni kodi ya pango,” amesema.
“Kodi
hii ni tangu mwaka 1998 haijawahi kulipwa, kulikuwa na kesi mahakamani
na Tanesco ikashinda na mahakama imeitaka kuondoka lakini mpaka sasa
haijachukua hatua zozote.”
Mbunge
huyo pia alihoji kitengo cha wizara hiyo kutenga Sh700 bilioni kwa
ajili ya mradi wa umeme wa Stiegler’s Gorge badala ya fedha hizo
kuzipeleka Rea (Wakala wa Umeme Vijijini) na Tanesco.
Monday, 21 May 2018
Serikali nchini Tanzania imeshauriwa kuchukua hatua za kisheria kwa wafugaji wanaobainika kuingiza mifugo yao katika hifadhi ya wanyama -Bunda
Serikali nchini Tanzania imeshauriwa kuchukua hatua
za kisheria kwa wafugaji wanaobainika kuingiza mifugo yao katika hifadhi ya wanyama
na mapori ya akiba badala ya kukamata na
kupiga mnada pasipo kufuata utaratibu stahiki.
Ushauri huo umetolewa hii leo na Musa Gedi Musa
Wakili wa kujitegemea ambae pia ni mwalimu kitaaluma,ambapo amedai hakuna
sheria ya nchi inayoruhusu wafugaji kuuziwa
mifugo yao kiholele isipokuwa ni kuchukuliwa hatua kwa kufikishwa mahakamani .
Amesema ni fedheha kuuzwa kwa shilingi elfu sabini
ng’ombe mwenye thamani ya shilingi laki sita.
Akizungumzia changamoto zinazowakabili wafugaji
kanda ya ziwa na hasa mkoani mara mwenyekiti wa chama cha wafugaji kanda ya
ziwa Mrida mshota amesema kuwa wafugaji wamekuwa kama wahalifu .
Akitolea mfano wa athari ambazo wafugaji wamepata na
takwimu mbalimbali za wafugaji
waliokamatiwa mifugo yao na kuuzwa kwa bei ya chini ikiwemo wilayani Serengeti amedai
zaidi ya ng’ombe 200 walikamatwa wilayani Serengeti na kuuzwa kwa bei ya chini
na kuongeza kuwa mfumo mzima wa mnada uligubikwa na rushwa.
Akatwa Koromeo Na Mumewe Kwa Wivu Wa Mapenzi
Mwanamke
mmoja aliyefahamika kwa jina la Mary Miyombo (32), mkazi wa Kata ya
Hombolo, Bwawani mkoani Dodoma amenusurika kufa baada ya kukatwa
koromeo na mumewe wake akiyejulikana kwa jina la Mgowela Anderson.
Chanzo
cha kisa hicho kilichotokea Mei 16, mwaka huu kinaelezwa ni wivu wa
kimapenzi ambapo inadaiwa mwanamke huyo alikutwa na mwanamume mwingine
ndipo mumewe akamjeruhi kwa kumkata na panga kwenye koromeo na kukimbia.
Akizungumza
kwa tabu huku akilia, Mary ambaye kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya
Rufaa ya Mkoa wa Dodoma amesema siku ya tukio akiwa ametoka kuuza
pombe kilabuni kijijini hapo alifika nyumbani kwake na kwenda anapoweka
fedha zake ambapo aligundua 1,000 haipo jambo lililosababisha kumuuliza
mume wake huyo.
“Nilipomuuliza
tu kama amechukua hiyo hela ndipo kipigo kilipoanza hadi kufikia hatua
ya kunikata na panga shingoni, yaani simtaki tena yule mwanamume kwani
hii ni mara ya tatu ananipiga na kunijeruhi na nimekuwa nikimsamehe
lakini kwa hili simtaki tena,” amesema Mary.
Mganga
Mfawidhi wa hiyo, Caroline Damian amethibitisha kumpokea mgonjwa huyo
hospitalini ambaye alilazwa wodi namba 10 na tayari amesharuhusiwa.
Hata hivyo, Kamanda wa polisi Mkoani Dodoma Gilles Muroto alipotafutwa kuzungumzia tukio hilo hakupatikana.
Askofu wa kkkt aliyepigwa mawe aibiwa kiti.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la
Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Njombe, Isaya Mengele, amesema kuwa
kitendo kilichofanywa na baadhi ya waumini wa kanisa hilo Dayosisi ya Ziwa Tanganyika
kumjeruhi kwa kumpiga mawe Askofu wa KKKT Dayosisi ya Tanganyika, Ambele
Mwaipopo,limelitia doa kanisa hilo na kinapaswa kulaaniwa.
Akizungumza jana katika ibada maalum
iliyofanyika katika Kanisa la Kiaskofu la KKKT Usharika wa Sumbawanga Mjini,
Askofu Mengele ambaye ni Mwenyekiti wa maaskofu wa KKKT Kanda ya Kusini,
alisema ni aibu kubwa na fedheha kwa dayosisi hiyo yenye miaka minne tangu
kuanzishwa kwake na waumini hao wanapaswa kutubu na kuomba radhi.
Alisema kuwa pia yeye ataongoza
ujumbe wa maaskofu wa kanda hiyo kwenda kwa Rais John Magufuli kumuomba radhi
kwa kitendo cha baadhi ya waumini hao kuvuruga amani ambayo serikali yake
imekuwa ikiihimiza kwa kitendo cha kumjeruhi kwa kumpiga mawe Askofu Mwaipopo.
Pia Askofu alimshauri Askofu
Mwaipopo kuvunja Baraza la Dayosisi hiyo kwa kuwa baadhi ya wajumbe wake
wamekuwa ni chanzo cha mgogoro uliopo katika kanisa hilo na wamekosa utii
kwake.
Muda mfupi kabla maaskofu sita
wanaounda Kanda ya Kusini ya KKKT hawajafika kuongoza ibada ya jana na kumpa
pole Askofu Mwaipopo kwa kujeruhiwa, baadhi ya waumini waliingia katika kanisa
hilo na kuondoa kiti maalum cha kukalia askofu huyo wakati wa kuongoza ibada.
Maaskofu hao ni Renald Mtenji wa
Ulanga Kilombero, Askofu Blastone Gaville (Dayosisi ya Dira-Iringa), Askofu Job
Mbwilo (Dayosisi ya Kusini Magharibi- Matamba), Askofu Amon Mwenda (Dayosisi ya
Ruvuma), Askofu Edward Mwaikali (Dayosisi ya Konde Mbeya) na Askofu Isaya
Mengele (Dayosisi ya Kusini Njombe).
Lengo la jopo hilo la maaskofu hao
limefika kumpa pole Askofu Mwaipopo na kuwasihi waumini waache mara moja
vitendo vya uvunjifu wa amani kwa kuwa vinaliumiza na kulichafua kanisa hilo
ambalo lina zaidi ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake nchini.
Katika ibada hiyo Katibu wa Dayosisi
ya Ziwa Tanganyika, Fredrick Lazaro, alisoma tamko maalum la Halmashauri Kuu
kwa wakristo wa Usharika wa Kathedral Sumbawanga Mjini kuekeleza waumini 21 na
watumishi wa kanisa hilo kuwa wamejitenga na kanisa hilo kwa muda usiojulikana.
Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa,
Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga, Dk. Alfan Haule, alisema vitendo vya uvunjifu wa
amani havitafumbiwa macho na serikali na kama vitaendelea, itatumia vyombo
vyake vya ulinzi na usalama kuvidhibiti.
Dk. Khaule aliagiza kuwa wote
walioiba kiti cha Askofu Mwaipopo wasakwe na wakamatwe, ili wafikishwe mbele ya
sheria wachukuliwe hatua kwani kitendo cha kuiba kiti hicho ni wizi kama wizi
mwingine wowote.
Mei 7, mwaka huu, Askofu Mwaipopo
alifukuzwa kwa mawe baada ya baadhi ya waumini kumzuia kuingia usharikani
wakidai hawataki kumuona akiwepo eneo la kanisa la Usharika wa Simbawanga
Mjini.
Subscribe to:
Posts (Atom)