Serikali nchini Tanzania imeshauriwa kuchukua hatua za kisheria kwa wafugaji wanaobainika kuingiza mifugo yao katika hifadhi ya wanyama -Bunda - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Monday 21 May 2018

Serikali nchini Tanzania imeshauriwa kuchukua hatua za kisheria kwa wafugaji wanaobainika kuingiza mifugo yao katika hifadhi ya wanyama -Bunda


Serikali nchini Tanzania imeshauriwa kuchukua hatua za kisheria kwa wafugaji wanaobainika kuingiza mifugo yao katika hifadhi ya wanyama na mapori ya akiba badala ya kukamata na  kupiga mnada pasipo kufuata utaratibu stahiki.

Ushauri huo umetolewa hii leo na Musa Gedi Musa Wakili wa kujitegemea ambae pia ni mwalimu kitaaluma,ambapo amedai hakuna sheria ya nchi  inayoruhusu wafugaji kuuziwa mifugo yao kiholele isipokuwa ni kuchukuliwa hatua kwa kufikishwa mahakamani .

Amesema ni fedheha kuuzwa kwa shilingi elfu sabini ng’ombe mwenye thamani ya shilingi laki sita.

Akizungumzia changamoto zinazowakabili wafugaji kanda ya ziwa na hasa mkoani mara mwenyekiti wa chama cha wafugaji kanda ya ziwa Mrida mshota amesema kuwa wafugaji wamekuwa kama wahalifu .
 
Akitolea mfano wa athari ambazo wafugaji wamepata na  takwimu mbalimbali za wafugaji waliokamatiwa mifugo yao na kuuzwa kwa bei ya chini ikiwemo wilayani Serengeti amedai zaidi ya ng’ombe 200 walikamatwa wilayani Serengeti na kuuzwa kwa bei ya chini na kuongeza kuwa mfumo mzima wa mnada uligubikwa na rushwa.



No comments:

Post a Comment