Wafanyabiashara katika soko la manjebe wamewalalamikia wafanyabiashara wenzao wanaopinga agizo la halmashauri-Bunda - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Thursday 17 May 2018

Wafanyabiashara katika soko la manjebe wamewalalamikia wafanyabiashara wenzao wanaopinga agizo la halmashauri-Bunda


Wafanyabiashara katika soko la manjebe wamewalalamikia wafanyabiashara wenzao wanaopinga agizo la halmashauri  ya mji  wa Bunda likiwataka wafanya biashara wa soko la Nyasura kuhamia manjebe kwa madai kuwa wanakwamisha biashara zao katika soko hilo.

Wakizungumza na mazingira fm kwa nyakati tofauti  wafanyabiashara katika soko la manjebe wamesema kuwa  serikali itilie mkazo tamko lake ili wafanyabiashara wajue kuwa soko ni moja tu pia wafanyabiashara hao wametaka hatua kali za kisheria  zichukuliwe dhidi ya wale watakao goma kuhamia manjebe.

Kwa upande wake Geofrey ambae ni mfanyabiashara wa samaki katika soko la manjebe amesema kuwa ametekeleza agizo la halimashauri ya mji lakini wale waliokiuka agizo hilo wamekuwa  wanasababisha hali ya kibiashara katika soko la manjebe kuwa mbaya zaidi.

Aidha Geofrey ametoa wito kwa kusema kuwa endapo wenzao waliopo soko la nyasura wakikataa kuhamia manjebe ameiomba serikali kuhamisha tena soko la Nyasura pamoja na soko la Manjebe kwenda ilikokuwa ofisi ya kijiji  kutokana na eneo hilo kuzungukwa na makazi ya watu na kuwa mzunguko mkubwa wa pesa. 


No comments:

Post a Comment