Saturday, 26 April 2025

Kiwango cha malaria mkoa wa Mara asilimia 15

 

Wito umetolewa kwa wananchi kuzingatia usafi wa mazingira na matumizi sahihi ya vyandarua ili kuepuka maambukizi ya malaria

Hayo yamesemwa leo na Dr Henry Lukamisa ambaye ni mratibu wa Malaria mkoa wa Mara wakati akizungumza kupitia Radio Mazingira fm ndani ya kipindi cha Asubuhi leo

Amesema hadi sasa kwa mkoa wa Mara kiwango cha ugonjwa wa malaria ni asilimia 15.

Dr Henry Lukamisa ambaye ni mratibu wa Malaria mkoa wa Mara

Dr Henry amesema ugonjwa wa malaria umeua watoto takribani 62 kwa mkoa wa Mara kwa mwaka 2024 kwa vifo vilivyorekodiwa hivyo ni vema wananchi wakachukua tahadhari

Dr Henry Lukamisa

Naye Mohamed Mlanza ambaye ni mratibu wa malaria halmashauri ya mji wa Bunda ambapo amesema kwa halmashauri hiyo wanajitahidi kutekeleza afua mbalimbali za kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa malaria ikiwa ni pamoja na kugawa vyandarua kwa mama wajawazito na kwa akina mama wenye watoto wachanga.

Mohamed Mlanza ambaye ni mratibu wa malaria

Aidha Mlanza ameongeza kuwa mbali na kutoa vyandarua pia idara hiyo inatoa elimu kwa jamii juu ya namna unavyoenezwa na kusambaa pamoja na madhara ugonjwa huo.

Mohamed Mlanza

Ikumbukwe kuwa kila tarehe 25 April kila mwaka Dunia huadhimisha siku ya malaria ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu ni ” Malaria inatokomezwa na sisi, wekeza chukua hatua, ziro malaria inaanza na mimi”

Wednesday, 23 April 2025

Mwalimu jela miaka 30 kwa ubakaji, ulawiti

 

Mbali na kifungo cha miaka 30 pia mahakama imeamuru kulipa fidia ya shilingi milioni 2 kwa muhanga kwa mujibu wa sheria ya uendeshaji wa makosa ya jinai 348 (1) sura ya 20 marejeo ya mwaka 2022.

Na Adelinus Banenwa

Mahakama ya wilaya ya Bunda imemuhukumu kifungo cha miaka 30 jela na fidia ya shilingi milioni 2 Vicent Joseph Nkunguu (39) aliyekuwa mwalimu mkuu wa shule msingi masaunga wilayani Bunda kwa kosa la ubakaji na ulawiti wa mwanafunzi (16) wa darasa la sita ambaye jina lake limehifadhiwa.

Hukumu hiyo ya kesi ya jinai namba 7623 ya mwaka 2024 imetolewa leo tarehe 23 April 2025 na hakimu mkazi mwandamizi wa mahakama ya wilaya ya Bunda mhe Betron Sokanya

Akisoma hukumu hiyo Mhe Sokanya amesema mahakama imejiridhisha bila kuacha shaka kuwa mtuhumiwa Vicent Joseph Nkungu alitenda kosa hilo baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili ambapo upande wa mashtaka uliwasilisha mashahidi watano (5) na kielelezo kimoja huku upande wa utetezi ukiwasilisha mashahidi wawili (2) bila kielelezo chochote.

Mhe Sokanya amesema katika kosa la kwanza la ubakaji mahakama imemtia hatiani kutokana na mshitakiwa huyo kutenda kosa angali akijua ni kinyume na kifungu cha 130 (1) (2)( e) na kifungu cha 131 (1) cha sheria ya kanuni ya adhabu sura 16 marejeo ya mwaka 2022

Aidha katika kosa la pili la kulawiti Mhe Sokanya amesema mahakama imemkuta mshitakiwa na hatia kinyume na kifungu cha cha 154 (1) (a) cha kanuni ya adhabu sura 16 marejeo ya mwaka 2022.

Mbali na kifungo cha miaka 30 pia mahakama imeamuru mshitakiwa Vicent kulipa fidia ya shilingi milioni 2 kwa muhanga kwa mujibu wa sheria ya uendeshaji wa makosa ya jinai 348 (1) sura ya 20 marejeo ya mwaka 2022.

Awali Mwendesha mashtaka wa serikali Isiaka Ibrahim Mohamed alisema matukio hayo yalitendeka tarehe 9 March 2024 nyumbani kwa mshitakiwa huku mwendesha mashtaka akiiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa ili liwe fundisho kwake na kwa wengine wenye tabia kama zake

Katika utetezi wake mshitakiwa aliiomba mahakama impunguzie adhabu kwa sababu ni mara yake ya kwanza kukutwa na hatia pia ana mke na watoto wanaomtegemea.

Mhe hakimu Sokanya amesema rufaa ipo wazi kwa hukumu hiyo.

Tuesday, 22 April 2025

Radio jamii zanolewa kumulika nafasi ya wanawake uchaguzi mkuu 2025

 

Picha ya pamoja washiriki wa mafunzo kwa radio jamii Tanzania yaliyotolewa na TAMWA kwa kushirikiana na TADIO jijiji Dodoma

Licha ya sensa ya watu na makazi ya 2022 kuonesha idadi ya wanawake ni wengi kuliko wanaume, katika nafasi za uongozi kwa ngazi za udiwani na ubunge bado kuna idadi ndogo zaidi ya uwakilishi.

By Edward Lucas

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania TAMWA kwa kushirikiana na TADIO wameendesha mafunzo kwa radio za kijamii Tanzania Bara kuandaa habari na vipindi vitakavyowawezesha wanawake kushiriki kikamilifu hasa kwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi mkuu wa 2025.

Akizungumzia mafunzo hayo, Meneja Mipango na Mikakati TAMWA, Sylivia Daulinge amesema mafunzo hayo yanayodhaminiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Vyombo vya Habari Finland VIKES yamelenga elimu ya namna bora ya kuandaa vipindi vya usawa na ujumuishi wa masuala ya kijinsia kwa kuhakikisha wanawake hasa vijana na makundi maalumu yanapewa kipaumbele kuelekea uchaguzi mkuu.

Sylivia Daulinge, Meneja Mipango na Mikakati TAMWA
Sylivia Daulinge, Meneja Mipango na Mikakati TAMWA

Kwa upande wake Mkufunzi wa mafunzo hayo kutoka Radio Tadio, Hilali Alexander Ruhundwa amesema kwa kushirikiana na TAMWA wameona wanajukumu la kufanya katika jamii kwa kuwashirikisha waandishi wa habari ili kufikisha elimu kwa jamii kuwafanya wanawake washiriki kikamilifu katika uchaguzi ujao

Hilali Alexander Ruhundwa, Mkufunzi wa mafunzo kutoka Radio Tadio akieleza kuhusu malengo ya mafunzo kwa radio za jamii kuelekea uchaguzi wa 2025
Sauti ya Hilali Alexander Ruhundwa

Kwa takwimu za uchaguzi mkuu uliopita wa mwaka 2020, madiwani wanawake waliochaguliwa kwenye kata ni 260 kati ya 3,953 ambao ni sawa na asilimia 6.58 na kwa upande wa ubunge kati ya majimbo 264 wabunge wanawake waliochaguliwa kwenye majimbo ni 26 tu sawa na asilimia 9.85

Wednesday, 16 April 2025

Nyamo-hanga azikwa leo kwao Bunda

 

Ni aliyekuwa mkurugenzi mtendaji wa TANESCO aliyefariki kwa ajali ya gari eneo la nyatwali Bunda

Na Adelinus Banenwa

Shughuli ya mazishi ya aliyekuwa mkurugenzi wa TANESCO Boniface Gissima Nyamo-hanga inaendelea nyumbani kwake Mtaa wa Migungani kata ya Bunda stoo Bunda mjini mkoani Mara .

Ibada ya Mazishi ikiongozwa na Askofu Mwita Maguge wa kanisa la kiinjiri la kirutheli Tanzania KKKT dayosisi mkoani Mara.

Katika ujumbe wake kwenye ibada hiyo askofu Mguge amesema hakuna mtu anayeweza kukikimbia kifo hata kama una ulinzi wa namna gani kifo kitakufuata.

Viongozi mbalimbali wamefika katika shughuli hizo zinaongozwa na Naibu waziri mkuu na waziri wa Nishati Mhe Dotto Biteko ambapo pia amesema tanesco na na taifa kwa ujumla limempoteza mtu muhimu sana ambaye mara zote alikuwa si mtu wa kulalamika bali akiona tatizo basi anatoa na njia ya kutatua tatizo hilo.

Akisoma wasifu wa marehemu Gissima Nyamo-hanga, Irene Gowele afisa mawasiliano TANESCO amesema Mhandisi Gissima alizaliwa tarehe 10 Sept 1969 mkoani Mara huku akishika nyadhifa mbalimbali za uongozi ikiwemo mkurugenzi mkuu wa REA  kati ya mwaka 2016 hadi 2019, wakala wa ujenzi Tanzania. TBA na baadae kuwa Mkurugenzi mtendaji wa TANESCO Tanzania ambapo hadi umauti alikuwa akitumika katika nafasi hiyo

Mhandisi Boniface Gissima Nyamo-hanga ameacha wajane wawili na watoto 15.

Ikumbukwe Mhandisi Nyamo-hanga alifariki dunia April 13, 2025 katika ajali ya gari eneo la Nyatwali Bunda

Friday, 21 March 2025

Diwani wa Ketare ambaye ni Mkurugenzi Radio Mazingira na atunukiwa hati ya Pongezi

 

Diwani wa kata ya Ketare Mhe Mramba Simba Nyamkinda akipokea hati ya pongezi kutoka kwa mwenyekiti wa CCM Bunda

viongozi hao wameonesha umoja na ushirikishanaji wa taarifa za miradi pindi inapopelekwa kwenye maeneo yao.

Na Adelinus Banenwa

Halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Bunda imewapongeza baadhi viongozi wilayani Bunda kwa utekelezaji na usimamizi wa miradi ya serikali kwenye maeneo yao.

Akizungumza katika kikao cha halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Bunda Mwenyekiti wa CCM wilaya, Abraham Mayaya Magese amesema viongozi hao wameonesha umoja na ushirikishanaji wa taarifa za miradi pindi inapopelekwa kwenye maeneo yao.

Wajumbe wa halmashauri ya wilaya kuu CCM wilaya ya Bunda

Akizungumzia mradi wa shule ya sekondari ya Nyaburundu iliyopo kata ya Ketare, Mayaya amesema kamati ya siasa baada ya kufika katika mradi huo ilikuta kuanzia viongozi wa kata mpaka wananchi wanataarifa zinazofanana kuhusu mradi huo.

Sauti ya Mwenyekiti wa CCM wilaya, Abraham Mayaya Magese

Miongoni mwa waliotunukiwa hati hizo za pongezi ni pamoja an Mhe Diwani wa Kata ya Ketare Mramba Simba Nyamkinda, mkuu wa shule ya msingi Nyaburundu, Mwenyekiti wa CCM kata ya Ketare, Diwani wa kata ya Nyasura Magigi Samweli Kiboko, miongoni mwa viongozi wengine.

Diwani wa kata ya Nyasura Magigi Samweli Kiboko akipokea hati ya pongezi kutoka kwa mwenyekiti wa CCM Bunda

Wakizungumza Mara baada ya kupokea hati hizo Diwani wa kata ya Ketare Mhe Mramba Simba Nyamkinda na diwani wa kata ya Nyasura Magigi Samweli Kiboko wamesema

Sauti za madiwani waliotunukiwa hati za pongezi

Wednesday, 19 March 2025

Wananchi watakiwa kuzingatia usafi kuepuka magonjwa ya mlipuko

 

Wananchi watakiwa kuzingatia usafi kuepuka magonjwa ya mlipuko

19 March 2025, 

Maafisa afya kutoka halmashauri ya mji wa Bunda

Kazi kubwa ya wataalamu ni kutoa elimu kwa jamii ili kudhibiti magonjwa ya milipuko kama vile kipindupindu, kichocho, miongoni mwa magonjwa mengine.

Na Adelinus Banenwa

Wito umetolewa kwa jamii kuzingatia usafi wa mazingira na vyakula ili kuepukana na magonjwa ya mlipuko ambayo ni hatari kwa afya za wananchi,

Hayo yamesemwa na maafisa afya kutoka halmashauri ya mji wa Bunda wakati wakizungumza kupitia kipindi cha Asubuhi leo kinachorushwa na radio Mazingira Fm.

Mohamed  Mlanza mratibu wa utoaji elimu ya afya kwa jamii kutoka halmashauri ya mji wa Bunda

Mohamed  Mlanza mratibu wa utoaji elimu ya afya kwa jamii kutoka halmashauri ya mji wa Bunda amesema kazi yao kubwa kama wataalamu ni kutoa elimu kwa jamii ili kudhibiti magonjwa ya milipuko kama vile kipindupindu, kichocho, miongoni mwa magonjwa mengine,

Akizungumzia ugonjwa wa homa ya nyani (M-POX) Mlanza amesema ugonjwa huo umeshatangazwa na serikali kwamba upo hivyo ni jukumu la wananchi kuchukua tahadhari endapo wataona dalili za ugonjwa huo ambazo ni pamoja na vipere sehemu za usoni, miguuni, mikononi , homa , maumivu ya kichwa miongoni mwa dalili zingine.

Sauti ya Mohamed  Mlanza mratibu wa utoaji elimu ya afya kwa jamii kutoka halmashauri ya mji wa Bunda
Amani Mashauri Jumbula, afisa afya halmashauri ya mji wa Bunda

Kwa upande wake Amani Mashauri Jumbula, afisa afya halmashauri ya mji wa Bunda amesema mbali na elimu inayotolewa lakini jukumu kubwa lipo kwa wananchi kuzingatia usafi hasa katika magonjwa kama kipindupindu chanzo chake ni uchafu hasa pale mtu anapokula chakula chenye vimelea vya wadudu wa kipindupindu ambao msingi wake ni kinyesi .

Ametoa wito kwa jamii kuzingatia kanuni zote za afya ikiwemo kunawa mokono, kuwa na vyoo bora , kuepuka kula vyakula ambavyo nivyabaridi miongoni mwa tahadhari zingine.

Sauti ya Amani Mashauri Jumbula, afisa afya halmashauri ya mji wa Bunda

Saturday, 15 March 2025

 

Bunda kuadhimisha miaka minne ya Rais Samia Machi 17

15 March 2025, 5:46 pm

Katibu tawala wilaya ya Bunda Ndugu Salumu Mtelela

Miongoni mwa maeneo yatakayoangaziwa ni pamoja na sekta mbalimbali za serikali ikiwemo Maji, Umeme, Afya, Barabara pamoja na Elimu.

Na Adelinus Banenwa

Serikali wilayani Bunda imewaomba wananchi wote kuudhuria maadhimisho ya miaka minne ya serikali ya awamu ya sita chini ya rais Samia Suluhu Hassan yanatarajiwa kufanyika Tarehe 17 March 2025.

Akizungumza na radio mazingira fm ofisini kwake katibu tawala wilaya ya Bunda Ndugu Salumu Mtelela amesema wananchi wote wanaalikwa siku hiyo ya jumatatu ambapo watapata nafasi ya kusikiliza kile serikali ya awamu ya sita imefanya ambapo mgeni rasmi atakuwa ni mkuu wa wilaya ya Bunda Mhe Aswege Enock Kamnyoge.

Sauti ya Katibu tawala wilaya ya Bunda Ndugu Salumu Mtelela

Aidha Mtelela amesema ratiba ya maadhimisho hayo inatarajiwa kuanza na zoezi la upandaji miti katika eneo la Kunzugu kisha kwenye viwanja vya ukumbi wa Maika na miongoni mwa maeneo yatakayoangaziwa ni pamoja na sekta mbalimbali za serikali ikiwemo Maji, Umeme, Afya, Barabara pamoja na Elimu.

Ameongeza kuwa katika kipindi cha miaka minne ya rais Samia wilaya ya Bunda imepokea kiasi cha fedha za miradi zaidi ya Bilion 247 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali.

Sauti ya Katibu tawala wilaya ya Bunda Ndugu Salumu Mtelela

Ikumbukwe Rais Samia Suluhu Hassan aliapishwa kuwa rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania mnamo March 19, 2021 baada ya kifo cha mtangulizi wake Hayati Dr John Pombe Magufuli Rais awamu ya tano.

Sunday, 9 March 2025

 

Mbunge Ghati ahimiza ushirikiano kwa wanawake

Mbunge viti maalumu mkoa wa Mara kutia kundi la wanawake Mhe Ghati Chomete

Mbali na kuwataka wanawake kuwa na mshikamano pia amesema ni lazima zisemwe kazi nzuri zilizofanywa na serikali awamu ya sita chini ya rais Samia Suluhu Hassan

Na Adelinus Banenwa

Wito umetolewa kwa wanawake wote kuwa na ushirikiano na kujenga tabia ya kupendana ili kutimiza adhma ya nafasi ya mwanamke katika jamii.

Hayo yamesemwa leo tarehe 7 March 2025 na mbunge viti maalumu mkoa wa Mara kupitia kundi la wanawake Mhe Ghati Chomete katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambapo kwa wilaya ya Bunda yamefanyika leo katika viwanja vya CCM wilaya ya Bunda.

Mbunge viti maalumu mkoa wa Mara kutia kundi la wanawake Mhe Ghati Chomete, Akiwa na mwenyekiti wa kamati ndogo ya fedha na uchumi CCM Bunda Ndugu Kambarage Wasira

Mbunge Chomete kama mgeni rasmi katika maadhimisho hayo wilayani Bunda mbali na kuwataka wanawake kuwa na mshikamano pia amesema ni lazima zisemwe kazi nzuri zilizofanywa na serikali awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kama vile miundombinu ya maji barabara, umeme elimu miongoni mwa kazi zingine.

Sauti ya mbunge viti maalumu mkoa wa Mara kutia kundi la wanawake Mhe Ghati Chomete
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Bunda Ndugu Abraham Mayaya Magese

Naye mwenyekiti wa CCM wilaya ya Bunda Ndugu Abraham Mayaya Magese amewapongeza wanawake kwa kuadhimisha siku yao huku akisema chama cha mapinduzi kinatambua mchango mkubwa unafanywa na wanawake viongozi wa chama cha mapinduzi na serikali huku akiwata viongozi hao kutatua kero za wananchi kila mmoja kwa eneo alilopo iwe ni ngazi ya mtaa au kijiji, Kata, mpaka wilaya.

Sauti ya mwenyekiti wa CCM wilaya ya Bunda Ndugu Abraham Mayaya Magese

Aidha viongozi hao wasemema kazi kubwa ya CCM ni kuangalia na kutatua kero za wananchi wakitolea mfano utatuzi wa migogoro baada ya tamko la hivi karibuni kuhusu mabasi kusitisha kushusha abiria katika vituo vya Nyasura na Bunda DDH ambapo kupitia viongozi hao wameeleza kuwa tayari malalamiko ya bodaboda na wajasiliamali yamefanyiwa kazi na mabasi yataendelea kushusha abiria katika vituo hivyo.

Sauti ya mwenyekiti wa CCM wilaya ya Bunda Ndugu Abraham Mayaya Magese

Miongoni mwa viongozi waliokuwepo kwenye Maadhimisho hayo ya siku ya wanawake Duniani ni pamoja na Mwenyekiti wa kamati ya fedha, mipango na uchumi chama cha mapinduzi wilaya ya Bunda Eng Kambarage Masatu Wasira ambaye amesema kuna kila sababu ya kuwapongeza wanawake kwa hatua kubwa ya kimaendeleo walizopiga

Kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani hufanyika March 8, ambapo kwa mwaka huu kitaifa yanatarajiwa kufanyika mkoani Arusha ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan

Thursday, 6 March 2025

 

Anusurika kifo baada ya kushambuliwa na mamba akioga

6 March 2025, 5:29 pm

Anusurika kifo baada ya kushambuliwa na Mamba alipokwenda ziwani asubuhi, rafiki apanda juu ya mamba kunusuru ndugu yake.

Na Adelinus Banenwa

Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina la Baraka Jumanne Maseke mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya sekondari Neruma kata ya Neruma halmashauri ya wilaya ya Bunda amenusurika kifo baada ya kushambuliwa na Mamba alipokwenda ziwani asubuhi.

Akizungumza na Mazingira fm mjomba wa kijana huyo aitwaye Exavely Palapala amesema tukio hilo limetokea asubuhi ya tarehe 5 March 2025 majira ya saa kumi na mbili asubuhi ambapo Baraka akiwa ameambatana na rafiki yake aitwaye Dotto Maingu Elias walikwenda ziwani kuoga ili kwenda shule.

Palapala ameongeza kuwa kwa mujibu wa maelezo yao baada kufika ziwani Baraka alikuwa wa kwanza kuingia kwenye maji ndipo alipo dakwa na mamba muda mfupi tu baada ya kuanza kuoga.

Sauti ya Exavely Palapala Mjomba wa Baraka,

Kwa upande wake Dotto Maingu aliyekuwa ameambatana na Baraka ameiambia Mazingira fm kuwa baada tu ya kufika ziwani Baraka alitangulia kuingia majini na yeye alibaki akiwa amekaa ufukweni.

Anasema baada ya muda mfupi tu alisikia kelele za rafiki yake akiwa kwenye maji akiomba msaada ndipo alipovua ngua haraka na kujitosa kwenye maji ili aone namna ya kumsaidia.

Sauti ya Dotto Maingu rafiki yake Baraka

Naye mwenyekiti wa kikiji cha Kasaunga ndugu Benard James Nyamwega amesema ni kweli taarifa za tukio hilo anazo na kuwa tukio hilo lilitokea jana lakini vijana hao hawakwenda kuoga bali kuangali mitego yao ya samaki ndipo mmojawapo akashambuliwa na mamba.

Sauti ya mwenyekiti wa kikiji cha Kasaunga ndugu Benard James Nyamwega

Baraka kwa sasa a anapatiwa matibabu katika Hospitali ya mkoa ya mwal Nyerere ya mkoani maarufu hospitali ya Kwangwa.

Tuesday, 4 March 2025

 

Mtoto Angel aliyezama kwenye rambo apatikana akiwa amefariki

4 March 2025, 

Kaimu kamanda wa zimamoto na uokoaji mkoa wa Mara Agostino Magere

Mwili wa mtoto huyo umeopolewa na askari wa zimamoto na uokoaji walikuwa eneo la tukio tangu March 2, 2025 walipopata taarifa za tukio hilo.

Na Adelinus Banenwa

Mtoto Angel Wilson 8 mwanafunzi wa darasa la pili shule ya msingi Kataryo B halmashauri ya Musoma Vijijini mkoani Mara aliyedaiwa kuzama kwenye bwana la maji amepatikana akiwa amefariki.

Kaimu kamanda wa zimamoto na uokoaji mkoa wa Mara Agostino Magere amesema mwili wa mtoto huyo umeopolewa leo na askari wa zimamoto na uokoaji walikuwa eneo la tukio tangu March 2, 2025 walipopata taarifa za tukio hilo.

Magere amesema chanzo cha tukio hilo ni kukosekana kwa umakini ambapo mtoto Angel Wilson akiwa na dada yake wa kidato cha tatu walikwenda kuchota maji ambapo maeneo hayo ni hatari kwa usalama hali iliyopelekea mtoto huyo kutereza na kuzama.

Sauti ya Kaimu kamanda wa zimamoto na uokoaji mkoa wa Mara Agostino Magere

Magere ametoa rai kwa wananchi kujenga tabia ya kulitaarifu jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Mara mapema pindi kunapohitajika maokozi ama ya moto au watu kuzama majini.