'KAMBARAGE WASIRA AWAUNGA MKONO CCM KATA YA MCHARO' - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Saturday 29 April 2023

'KAMBARAGE WASIRA AWAUNGA MKONO CCM KATA YA MCHARO'

 



Mwenyekiti wa kamati ndogo ya fedha, uchumi na mipango ccm wilaya ya Bunda, Kambarage Masatu Wasira amechangia mabati 64 yenye thamani ya shilingi mil 1.7 kwa ajili ya uendelezaji na ukamilishaji wa ujenzi ofisi ya ccm kata ya Mcharo. 

Akizungumza wakati wa kukabidhi mabati hayo jana tarehe 28 April 2023 amesema katika kata hiyo kuna changamoto ya upatikanaji wa vifaa vya ujenzi wa ofisi ya ccm ambayo ina takribani miaka 4 tangu kuanza ujenzi huo lakini mpaka sasa bado haujakamilika.

"Mwenyekiti wa CCM Mkoa Mh Chandi Marwa aliwaahidi kuwapa shilingi laki 5 lakini pia kwa ujio wetu huu tumeweza kupata wadau pia wamechangia zaidi ya laki 5 ya kusaidia misumali na vitu vingine ili shughuli iendelee na mbao zitaingia siku ya jumatatu kutoka kwa Kazi mfanyabiashara wa Mwanza ambaye naye amejitoa kuchangia" amesema Kambarage Wasira.



Kambarage Masatu Wasira akikabidhi mabati kwa ajili ya ujenzi ofisi ya ccm kata ya mcharo

Kwa upande wake Mwenyekiti CCM kata ya Mcharo, Ndugu Phinias Kasoga amesema kutokana na ukosefu wa ofisi wamekuwa na mazingira magumu katika utekelezaji wa majukumu yao mfano utunzaji wa nyaraka za chama na kwamba kukamilika kwa jengo hilo kutaongeza ufasi wa kazi.

"Tumekuwa na mazingira magumu kidogo kwasababu ofisi ambayo tumekuwa tukiitumia katika masuala yetu ni ofisi ya tawi ambapo unakuta ofisi moja imebeba mamlaka nyingi wakati mwingine amani ilikuwa haikai vizuri au utunzaji wa kumbukumbu za kichama umekuwa na changamoto sana" amesema Phinias Kasoga. 



Picha ya Jengo la ofisi za CCM kata ya Mcharo lililopo mtaa wa Changuge ambalo linawekewa mipango ya kukamirishwa


Mabati 'bando 4' yaliyotolewa na Mwenyekiti wa kamati ndogo ya fedha, uchumi na mipango CCM wilaya ya Bunda, Kambarage Masatu Wasira yakikabidhiwa kwa uongozi wa CCM kata ya Mcharo.





Baadhi ya wanachama na viongozi wa CCM kata ya Mcharo wakiwa katika mazungumzo kabla ya zoezi la kukabidhi mabati lilolofanyika katika eneo la Changuge


No comments:

Post a Comment