Baba amlawiti mwanaye ili kuinua huduma yake ya M-pesa kijiji cha Mwibagi Wilaya ya Butiama - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Sunday 16 April 2023

Baba amlawiti mwanaye ili kuinua huduma yake ya M-pesa kijiji cha Mwibagi Wilaya ya Butiama

 

Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Butiama, Atula Pascal Sanga

Baba amlawiti mwanaye ili kuinua huduma yake ya M-pesa huku wengine wakifanya vitendo vya ubakaji kwa imani za kishirikina kwa lengo la kupata dhahabu katika machimbo.


Hayo yamebainishwa na Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Butiama, Atula Pascal Sanga wakati wa Kongamano la kuadhimisha siku ya kuzaliwa Hayati Baba wa Taifa Mwl Nyerere lililofanyika katika viwanja vya Kituo cha Makumbusho ya Mwl Nyerere Butiama Mkoani Mara tarehe 15 April 2023.


Akiwasilisha mada kuelezea uzoefu wa kulinda na kutetea haki za wanawake na watoto katika Wilaya hiyo, Sanga amesema licha ya mafanikio mbalimbali katika juhudi za kukabiliana na vitendo vya ukatili kumekuwa na mila na destori potofu katika imani za kishirikina zinazochangia kuwepo kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia wilayani humo.https://www.instagram.com/p/CrF0FXIOFuM/






















No comments:

Post a Comment