Watu Watatu wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za mauaji -Bunda Mara - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Thursday 19 April 2018

Watu Watatu wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za mauaji -Bunda Mara


Jeshi la polisi wilaya ya Bunda Mkoani Mara linawashikilia Watu watatu kwa tuhuma za mauwaji ya mwanamkea mmoja aliyetambuliwa  kwa jina la  Bhoke mke wa matasu mwenye umri wa miaka 64 mkazi wa kijiji cha kyandege kata ya mgeta.

Tukio la kuuwawa kwa mwanamke huyo limetokea alfajiri ya tarehe 16 mwezi huu wakati mwanamke huyo akitoka chooni kujisaidia ndipo alipigwa na wauwaji hao na kitu chenye ncha kali sehemu za mgongoni na shingoni.

Baada ya  kutekeleza mauaji hayo watu hao hawakuchukuwa kitu chochote kutoka kwa marehemu licha ya marehemu kuwa na fedha kiasi cha shilingi laki moja ambapo imeelezwa kuwa chanzo cha mauji hayo ni imani za kishirikina.

Hata hivyo Jeshi la polisi wilaya ya bunda limetoa wito kwa wananchi kutoa taarifa mapema pindi wanapoona hali kama hiyo ndani ya jamii.

No comments:

Post a Comment