Wachezaji hawa uwenda wakaondoka Man United mwisho wa msimu huu - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Thursday 19 April 2018

Wachezaji hawa uwenda wakaondoka Man United mwisho wa msimu huu


Mtandao wa Squawka.com moja kati ya stori kubwa walioiripoti leo Alhamisi ya April 19 2018 ni pamoja na hii ya wachezaji wa Man United ambao wanatazamiwa kuwa wataondoka mwisho wa msimu kwa sababu mbalimbali ikiwemo kukosa nafasi ya kucheza.

1- Anthony Martial ametajwa kuwa ataondoka Man United baada ya kugoma kusaini mkataba mpya wa miaka mitano kutokana na kocha Jose Mourinho kutomchezesha mara kwa mara, hivyo vilabu vya Juventus na Inter Milan vimekuwa vikihusishwa nae kwa karibu, Martial ameanza katika game 16 tu za Man United msimu huu na nafasi yake amekuwa akipewa Rashford.

2- Paul Pogba pamoja na kuwa amenunuliwa kwa pesa nyingi kutoka Juventus na kujiunga na Man United na amefanikiwa kutoa assist nyingi zaidi ya mchezaji yoyote wa Man United katika EPL lakini amekuwa anafanya vizuri kiasi chini ya Jose Mourinho na kuna wakati watu walihoji namna ya Mourinho anavyomtumia kiungo huyo.

3- Marouane Fellaini huyu alikuwa moja kati ya wachezaji wanaopendwa sana na Jose Mourinho msimu uliyoisha lakini maisha yake Man United yanadaiwa kama kukaribia mwisho baada ya kufanikiwa kucheza katika game 19 pekee za mashindano yote msimu huu huku akianza katika game tano pekee na amecheza kwa jumla ya dakika 694.

4- Ander Herrera baada ya ujio wa Nemanja Matic ndani ya Man United Herrera ameonekana kuanza kukosa nafasi ya kucheza na amepata kuanza katika game 10 za Man United, hivyo uwepo wa wachezaji wanatajwa kumzidi uwezo kunaweza kumfanya akakimbia Man United na kwenda timu ambayo atapata nafasi ya kucheza.

5- Luke Shaw anatajwa kuwa yeye mwenyewe ameanza kuhisi kuwa hana nafasi tena ndani ya kikosi cha Man United kutokana na nafasi  yake kuwa kuna kiungo kama Ashley Young wameanza kucheza hiyo inatokana na jeraha lake la muda mrefu alilolipata msimu uliyopita hivyo anakosa nafasi pia kutokana na kukosa fitness.

No comments:

Post a Comment