Thursday, 19 April 2018

Mkwasa aionya Simba


Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa amesema wao hawana hofu hata kidogo na mechi dhidi ya watani wao Simba.

Simba itakutana na Yanga katika mechi ya Ligi Kuu Bara itakayopigwa Aprili 29 jijini Dar es Salaam.

Mkwasa amesema anaamini kama ni maneno, basi watani wao Simba wangekuwa na nafasi ya kuwa mabingwa kwa kuwa “wanachonga” sana.

“Suala la kutishia kutufunga ni hadithi tu, mpira hauko hivyo. Unajua wenzetu wanaongea sana, maana kama ingekuwa kuna kombe la kuzungumza, basi wao wangekuwa mabingwa.

“Tuna timu nzuri na tunaweza kupambana na kufanya vizuri, hakuna masuala ya kusema utafungwa na mwingine kujiamini kwa asilimia mia atashinda,” alisema.

Mashabiki wa Simba ndiyo walikuwa wanatamba kwa muda mrefu kutokana na kasi ya kikosi chao katika Ligi Kuu Bara, lakini Yanga wamepata morali baada ya kikosi chao kuingia katika hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa kuing’oa Wolayta Dicha ya Ethiopia.

King Mswati abadilisha jina la nchi yake


Mfalme wa Swaziland, King Mswati III ametangaza kubadili jina la nchi hiyo na sasa itaitwa Kingdom of eSwatini ikimaanisha Ufalme wa eSwatini.

Mfalme huyo ametangaza mabadiliko ya jina hilo rasmi katika maadhimisho ya sherehe za miaka 50 ya Uhuru wa Swazi.

Sherehe hizo pia zimeadhimisha miaka 50 ya mtawala huyo ya kuzaliwa. Taifa hilo lililoko kusini mwa Afrika ni taifa lililo kwenye utawala kamili wa Kifalme.

Mfalme huyo anayejulikana kwa jina la Ngwenyama au “Simba”, anajulikana kwa kuwa na wake wengi na uvaaji wake wa kitamaduni.

Beki wa Chelsea afungiwa


Chama cha soka England FA leo kimetangaza maamuzi mazito kwa beki wa kimataifa wa Hispania anayeichezea Chelsea ya England Marcos  Alonso baada ya kukutwa na hatia ya kosa la kumchezea faulo ya makusudi mchezaji wa Southampton Shane Long.

FA leo wametangaza kuamua kumfungia mechi tatu Marcos Alonso baada ya kumkuta na hatia na kugundua kuwa Marcos alifanya kwa makusudi kumkanyaga Shane Long na kukusudia kumuumiza, kabla ya adhabu hiyo kutolewa Marcos alipewa muda hadi jana Jumatano ya  April 18 saa 20:00 ajitetee kwa nini asiadhibiwe.

Beki wa Chelsea Marcos Alonso aliingia matatizoni Jumamosi ya April 14 2018 katika mchezo kati ya Chelsea dhidi ya Southamton uliyomalizika kwa Chelsea kupata ushindi wa magoli 3-2, baada ya kumchezea faulo  Shane Long.

Wachezaji hawa uwenda wakaondoka Man United mwisho wa msimu huu


Mtandao wa Squawka.com moja kati ya stori kubwa walioiripoti leo Alhamisi ya April 19 2018 ni pamoja na hii ya wachezaji wa Man United ambao wanatazamiwa kuwa wataondoka mwisho wa msimu kwa sababu mbalimbali ikiwemo kukosa nafasi ya kucheza.

1- Anthony Martial ametajwa kuwa ataondoka Man United baada ya kugoma kusaini mkataba mpya wa miaka mitano kutokana na kocha Jose Mourinho kutomchezesha mara kwa mara, hivyo vilabu vya Juventus na Inter Milan vimekuwa vikihusishwa nae kwa karibu, Martial ameanza katika game 16 tu za Man United msimu huu na nafasi yake amekuwa akipewa Rashford.

2- Paul Pogba pamoja na kuwa amenunuliwa kwa pesa nyingi kutoka Juventus na kujiunga na Man United na amefanikiwa kutoa assist nyingi zaidi ya mchezaji yoyote wa Man United katika EPL lakini amekuwa anafanya vizuri kiasi chini ya Jose Mourinho na kuna wakati watu walihoji namna ya Mourinho anavyomtumia kiungo huyo.

3- Marouane Fellaini huyu alikuwa moja kati ya wachezaji wanaopendwa sana na Jose Mourinho msimu uliyoisha lakini maisha yake Man United yanadaiwa kama kukaribia mwisho baada ya kufanikiwa kucheza katika game 19 pekee za mashindano yote msimu huu huku akianza katika game tano pekee na amecheza kwa jumla ya dakika 694.

4- Ander Herrera baada ya ujio wa Nemanja Matic ndani ya Man United Herrera ameonekana kuanza kukosa nafasi ya kucheza na amepata kuanza katika game 10 za Man United, hivyo uwepo wa wachezaji wanatajwa kumzidi uwezo kunaweza kumfanya akakimbia Man United na kwenda timu ambayo atapata nafasi ya kucheza.

5- Luke Shaw anatajwa kuwa yeye mwenyewe ameanza kuhisi kuwa hana nafasi tena ndani ya kikosi cha Man United kutokana na nafasi  yake kuwa kuna kiungo kama Ashley Young wameanza kucheza hiyo inatokana na jeraha lake la muda mrefu alilolipata msimu uliyopita hivyo anakosa nafasi pia kutokana na kukosa fitness.

Achunwa ngozi ya uume..wachunaji waondoka nayo kahama- shinyanga


Mkazi mmoja wa kijiji na kata ya Kinaga, Kahama mkoani Shinyanga amechunwa ngozi ya sehemu za siri baada ya kuleweshwa kwa pombe.

Watu waliomchuna mkazi huyo anayejulikana kwa jina la Paschal Misana, wametoweka na hadi sasa hawajajulikana.

Diwani wa kata hiyo, Mary Manyambo alisema tukio hilo lilitokea Aprili 16, baada ya Misana kupigiwa simu na mtu aliyekuwa akimdai Sh200,000.

“Lakini kwa maelezo ya muathirika ni kuwa baada ya kufika nyumbani kwa mtu huyo alinyweshwa pombe hadi akapoteza fahamu na alizinduka asubuhi ya siku iliyofuata, akajikuta amechunwa uume wake kuanzia kwenye korodani,” alisema Manyambo.

Mganga wa zamu katika Hospitali ya Mji wa Kahama, Dk Abdallah Simba alisema jana kuwa mtu huyo alifikishwa hapo juzi mchana akiwa na hali mbaya.

“Aliletwa hapa sehemu yake ya uume ilikuwa imekatwa kwa kuzunguka na kisha kunyofolewa ngozi yote ya sehemu hizo hali iliyosababisha kuvuja damu nyingi,” alisema.

“Wachunaji hao walimkata kitaalamu kwani hawakufika kwenye mishipa ya sehemu za siri na hivyo tayari ameshonwa na kurudishiwa alipokuwa amekatwa wakati wa kuchunwa.

“Sehemu zake za siri zinaweza kuendelea kufanya kazi kama kawaida kwa sababu sehemu za mishipa hazikukatwa.”

Akizungumzia tukio hilo akiwa hospitalini hapo anapoendelea na matibabu, Misana alisema baada ya kupigiwa simu hiyo alikwenda kwa lengo la kulipwa fedha alizokuwa amemkopesha mtu huyo.

“Nilimkopesha ng’ombe mmoja kwa thamani ya Sh200,000 na nilipofika baiskeli yangu iliingizwa chumbani na kisha nikakaribishwa ndani,” alisema.

Misana alisema baada ya kukaa, aliwaona wageni watatu waliokuwa chumbani, wawili wakiwa wanawake.

Alisema baadaye alitengewa ugali ambao alikula na wenyeji na baada ya kumaliza alipewa pombe aina ya shujaa waliyokuwa wakipewa pia wageni wengine.

Majeruhi huyo alisema baada ya kunywa pombe hiyo alipoteza fahamu mpaka asubuhi alipozinduliwa na mke wa mtuhumiwa.

Hata hivyo, alisema alishangazwa na kitendo cha kuwa peke yake akiwa uchi, huku akitokwa damu na sehemu zake za siri zikiuma.

“Sikujua chochote, baada ya watu kujaa wasamaria wema na kuanza kunipa huduma ya kwanza, walinieleza kuwa sehemu zangu za siri zilikuwa zimekatwa, hali iliyonishtua na baadaye polisi walifika wakanichukua na kunipeleka hospitalini,” alisema.

Kamanda wa polisi wa mkoa, Simon Haule alisema tayari wanamshikilia mtuhumiwa kwa ajili ya mahojiano.

Baada ya kuhojiwa, mtuhumiwa huyo alisema wageni wake watatu walihusika kumchuna ngozi Misana na kutoweka nayo na mpaka alipokamatwa hajui walielekea wapi.

Polisi wanaendelea kuwasaka wageni hao huku mtuhumiwa akiendelea kusaidia upelelezi.