WWF yashirikiana na wadau kupima maji mto Tigite- Tarime - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Tuesday 26 September 2023

WWF yashirikiana na wadau kupima maji mto Tigite- Tarime

 

mtaalam kutoka shirika la WWF akiwa katika hatua ya kupimaubora wa maji. Picha na Thomas Masalu

Shirika la WWF kwa kushirikiana na bonde la ziwa Victoria wamefanya zoezi la kupima maji ya mto Tigite uliopo Kijiji cha Matongo Kata ya Matongo wilaya ya Tarime ili kubaini afya ya mto huo katika vigezo vya asili na vya kisayansi.

Na Thomas Masalu

Shirika la WWF kwa kushirikiana na bonde la ziwa Victoria wamefanya zoezi la kupima maji ya mto Tigite uliopo Kijiji cha Matongo Kata ya Matongo wilaya ya Tarime ili kubaini afya ya mto huo katika vigezo vya asili na vya kisayansi.

Zoezi hilo limefanyika leo 26 Sept 2023 ambapo limeshirikisha wadau mbalimbali kama vile vikundi vya watumia maji, wapimaji wa afya ya mto ngazi ya jamii, wanafunzi wa shule ya secondary Matongo na baadhi ya walimu wa shule hiyo.

wadau wakiwa katiaka hatua za upimaji wa maji, Picha na Thomas Masalu

Zoezi lilianza kwa wadau kupewa elimu katika kutambua umuhimu wa upimaji wa maji ya mto, afya ya mto na vifaa vinayotumika kupimia maji ya mto.

Pamoja na hayo wadau walionyeshwa hatua ya kwanza ya upimaji hadi hatua ya mwisho ya upimaji hali iliyo onyesha kufurahiwa na wadau kutokana na kupata maarifa mapya katika utuzanji wa vyanzo vya maji.

No comments:

Post a Comment