Mazingira Fm Nikituo Cha Radio Kiliopo Wilayani Bunda Mkuoni Mara,
Sunday, 16 February 2025
Wagonjwa 1,520 wahudumiwa bure katika kambi ya macho Bunda
16 February 2025,
rais wa Chama cha Lions Clubs International, Mahamoud Rajuan,
Zaidi ya Wagonjwa 1,520 Wahudumiwa Bure Katika Kambi ya Matibabu ya Macho Bunda Manyamanyama.
Na Adelinus Banenwa
Zaidi ya wagonjwa 1,520 wa macho wamehudumiwa ndani ya siku mbili kati ya tatu katika kambi maalumu ya matibabu ya macho iliyofanyika katika Hospitali ya Bunda Manyamanyama.
Akizungumza katika kambi hiyo, rais wa Chama cha Lions Clubs International, Mahamoud Rajuan, amesema kati ya wagonjwa hao, 150 wamefanyiwa upasuaji wa macho kutokana na changamoto mbalimbali walizokuwa nazo, ikiwa ni pamoja na mtoto wa jicho.
Baadhi ya wagonjwa waliopata huduma katika kambi ya macho ikiwemo kufanyiwa upasuaji
Mahamoud amewashukuru wananchi kwa kujitokeza na pia kuwashukuru wafadhili waliowezesha kufanyika kwa kambi hiyo, ambapo huduma zilikuwa bure.
Sauti ya rais wa Chama cha Lions Clubs International, Mahamoud Rajuan,Dr. Majey Majey, mganga anayehusika na huduma za matibabu ya macho
Naye, Dr. Majey Majey, mganga anayehusika na huduma za matibabu ya macho na vipimo, amesema kwa siku hizo mbili wamewahudumia wagonjwa 1,520 na wanashukuru wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kupata matibabu.
Dr. Majey ameeleza kuwa matatizo ya macho yanaweza kusababishwa na changamoto mbalimbali, ikiwemo aleji, mtoto wa jicho, presha ya macho, vumbi, moshi, na mengine, na hivyo wanatoa ushauri kulingana na chanzo cha ugonjwa wa kila mgonjwa.
Sauti ya Dr. Majey Majey, mganga anayehusika na huduma za matibabu ya machoBaadhi ya wagonjwa waliopata huduma katika kambi ya macho ikiwemo kufanyiwa upasuaji
Kwa upande wao, baadhi ya wagonjwa waliopata huduma katika kambi ya siku tatu wamewashukuru kwa huduma walizopata, kwani hawakudaiwa fedha yoyote kuanzia kwenye vipimo hadi upasuaji.
Kambi hiyo ya matibabu ya macho katika Hospitali ya Bunda Manyamanyama ilianza tarehe 14 Februari na kumalizika leo, tarehe 16 Februari 2025, huku matibabu yaliyotolewa ikiwa ni pamoja na huduma za vipimo, ugawaji wa miwani ya jua na kusomea, pamoja na upasuaji, yote hayo yakitolewa bure.
Saturday, 15 February 2025
Wavamia mtaa wa Zanzibar kufuatia kugunduliwa kwa dhahabu, serikali yatia mguu
15 February 2025,
Baadhi ya wananchi waliojikusanya kwenye eneo ilipoibuka rashi ya dhahabu
Serikali ya mtaa inachukua hatua muhimu katika kusimamia usalama na ustawi wa jamii katika kipindi hiki cha shughuli za uchimbaji.
Na Adelinus Banenwa
Makumi kwa mamia ya vijana kutoka maeneo mbalimbali wameshukudiwa katika viunga vya mtaa wa Zanzibar , kata ya Nyasura, halmashauri ya mji wa Bunda, kutokana na kuibuka kwa rashi ya madini ya dhahabu katika eneo hilo kwa lengo la kuanza shughuli za uchimbaji.
Mwenyekiti wa mtaa wa Zanzibar, Nyabatuli Ndege, amesema kuwa serikali ya mtaa inachukua hatua muhimu katika kusimamia usalama na ustawi wa jamii katika kipindi hiki cha shughuli za uchimbaji.
Baadhi ya wananchi waliojikusanya kwenye eneo ilipoibuka rashi ya dhahabu
Nyabatuli amesema kuwa wanahakikisha kuwa kuna usafi, maeneo ya chakula yamewekwa mbali na maeneo ya uchimbaji, na uchimbaji wa vyoo umeanzishwa ili kudumisha afya na usalama kutokana na wingi wa watu wanaokusanyika.
Sauti ya Mwenyekiti wa mtaa wa Zanzibar, Nyabatuli Ndege
Naye mtendaji wa mtaa wa Zanzibar, Bi. Grece Mwita, ameeleza kuwa halmashauri tayari imeanza kukusanya mapato kutoka kwa wachimbaji, ambapo kila kiroba cha mchanga kinachopakiwa kinatozwa shilingi 1000.
Baadhi ya wananchi waliojikusanya kwenye eneo ilipoibuka rashi ya dhahabu
Grece amesisitiza kuwa ni muhimu kwa wachimbaji kufuata utaratibu wa kisheria na kulipa mapato kwa mujibu wa sheria.
Sauti ya mtendaji wa mtaa wa Zanzibar, Bi. Grece Mwita
Aidha, Maiga James Majanjala, mwenyekiti wa wachimbaji wadogo wa madini wi, ametoa wito kwa vijana wote kuwa watulivu na kuzingatia sheria za uchimbaji. Huku akiwahakikishia kuwa viongozi wa wachimbaji wako mstari wa mbele kuhakikisha utaratibu unafuatwa ili kuepuka migogoro na madhara yoyote.
Sauti ya
Awali akizungumza na Mazingira fm moja ya vijana wa mwanzo kugundua uwepo wa dhahabu katika eneo hilo la Zanzibar amesema eneo hilo kwa kawaida walikuwa wanalitumia kuchimba kokoto na molamu lakini siku ya ijumaa jioni ndipo walipoona mawe yenye chembechembe za madini ya dhahabu na walipokwenda kuyasaga alipata gram 3.5 ndipo alianza kuwapa taarifa wengine
Sauti ya Mangaro Stima moja ya vijana wa mwanzo kugundua uwepo wa dhahabu
Friday, 14 February 2025
Radio Mazingira FM yapongezwa kwa utendaji kazi mzuri
14 February 2025,
Mkuu wa wilaya ya Musoma Juma Chikoka alipokuwa akizungumzia siku ya radio,(picha na Shomari)
Mkuu huyo wa wilaya ya Musoma amekipongeza kituo cha redio cha Mazingira Fm cha mjini Bunda kwa kazi nzuri za kuendelea kuwafikishia wananchi taarifa mbalimbali.
Na.Shomari Binda
Katika kuadhimisha siku ya radio duniani jamii imetakiwa kufatilia matangazo yake ili kuweza kupata taarifa mbalimbali zikiwemo za utekelezaji wa miradi ya serikali.
Kauli hiyo imetolewa februari 13,2025 na mkuu wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka alipokuwa akiizungumzia siku hiyo.
Amesema redio ni chombo muhimu na kinachopaswa kufatiliwa hivyo wananchi wanakumbushwa kufatilia matangazo yanayotolewa
Chikoko amesema ipo miradi inayotekelezwa na serikali katika Wilaya ya Musoma na maeneo mengine ya nchi na moja ya vyanzo vya kupata taarifa ni kupitia redio
Mkuu huyo wa Wilaya ya Musoma amekipongeza kituo cha redio cha Mazingira Fm cha mjini Bunda kwa kazi nzuri za kuendelea kuwafikishia wananchi taarifa mbalimbali.
Chikoka kupitia siku hii ya redio duniani amewapongeza watangazaji wa Mazingira Fm kwa kazi wanayoifanya ya kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata taarifa
Wednesday, 12 February 2025
Wanahabari wapigwa msasa uandishi bila kuleta taharuki
12 February 2025,
Ili kuwezesha jamii isipate madhara zaidi ni wajibu wa mwandishi wa habari na chombo cha habari kujua namna ya mbinu sahihi za kutumia ili kuleta matokeo chanya ambayo pia hayawezi kuleta taharuki kwenye jamii husika.
Na Adelinus Banenwa
Waandishi wa habari wa redio za kijamii wajengewa uwezo wa namna bora ya kuandika habari na kuandaa vipindi vya afya ambavyo haviwezi kusababisha taharuki kwa jamii ila kutoa elimu na uelewa.
Baadhi ya washiriki wa semina wakiendelea na mafunzo ya mbinu sahihi za uandaaji wa habari
Hayo yamejili leo Feb 11, 2025 ikiwa ni siku ya pili ya semina ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari kutoka redio za kijamii kanda ya ziwa kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa Marburg chini ya Ufadhili wa Shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia masuala ya watoto UNICEF
Prosper Laurent Kwigize mwandishi wa habari na mchambuzi wa masuala ya utatuzi wa migogoro moja kati ya watoa mada amesema ili kuwezesha jamii isipate madhara zaidi ni wajibu wa mwandishi wa habari na chombo cha habari kujua namna ya mbinu sahihi za kutumia ili kuleta matokeo chanya ambayo pia hayawezi kuleta taharuki kwenye jamii husika.
Washiriki wakiendelea kupata uzoefu wa uandaaji wa habari za afya
Ndugu proper amesema kuwa mara nyingi kwenye changamoto za magonjwa hasa ya milipuko yanapotokea watu wanataka kujua je vyombo vya habari vinasema nini hivyo ni wajibu wa chombo cha habari au mwanahabari mwenyewe kuseti ajenda ambayo kupitia maswali yake yanaweza kusaidia kutoa mwelekeo kwa jamii kuhusu ugonjwa husika.
Bunda: Shule kukosa mwalimu wa kike, DC atoa maagizo mazito
12 February 2025,
Dr Vicent Naano Anney, DC Bunda akizungumza katika baraza la madiwani halmashauri ya wilaya (Picha na Edward Lucas)
Kati ya walimu 350 waliopo halmashauri ya wilaya ya Bunda walimu wa kike ni 45 pekee.
Na Edward Lucas
Kutokana na kilio cha kukosa mwalimu wa kike shule ya sekondari Tirina, mkuu wa wilaya ya Bunda, Dr Vicent Naano Anney amempa siku moja mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo awe amempa barua ya kuonesha mwalimu amepelekwa katika shule hiyo
Naano ametoa maagizo hayo leo kupitia mkutano wa baraza la madiwani kupokea taarifa mbalimbali ya robo ya pili ya mwaka wa fedha 2024/2025 katika halmashauri ya wilaya ya Bunda
George Stanley Mbilinyi, DED halmashauri ya wilaya ya Bunda akiwa katika mkutano wa Baraza la Madiwani (Picha na Edward Lucas)
Awali akizungumzia changamoto hiyo diwani wa kata ya Mugeta, Mganga Jongora amesema shule ya sekondari Tirina ina wanafunzi wa kike na wa kiume lakini toka shule hiyo ifunguliwe haina mwalimu wa kike jambo linalosababisha wanafunzi wa kike wakose mtu wa kumfikishie changamoto zao
Sauti ya Mganga Jongora, Diwani wa Mugeta
Katika mahojiano na Mazingira Fm, Kaimu Afisa Elimu Sekondari wa halmashauri ya wilaya ya Bunda, Nambua Godfrey Semlugu amekiri kuwepo changamoto ya uhaba wa walimu wa kike kwani kati ya walimu 350 wa kike ni 45 pekee.
Sauti ya Nambua G. Semlugu
Dkt. Naano: Safari hii kwenye bajeti Bunda DC lipeni madeni ya watu
13 February 2025,
Dr Vicent Naano Anney, DC Bunda akizungumza katika baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya Bunda (Picha na Edward Lucas)
Halmashauri ya wilaya ya Bunda yatakiwa mwaka huu kwenye bajeti kutenge fedha kwa ajili ya kulipa madeni ya wadau mbalimbali.
By Edward Lucas.
Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Dr Vicent Naano Anney amemwagiza mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Bunda mwaka huu kwenye bajeti watenge fedha kwa ajili ya kulipa madeni ya wadau mbalimbali
Amesema ni aibu kuona watu wanajitokeza mara kwa mara wakidai pesa zao katika halmashauri ambazo waliingia nazo mikataba na kutoa tahadhari kwa miradi mipya inayotekelezwa awamu hii kuingia katika madeni
Sauti ya Dr.Vicent Naano, DC Bunda
Naano ameyasema hayo katika mkutano wa baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya Bunda lililofanyika jana tarehe 12 Feb 2025 kupokea taarifa ya robo ya pili ya mwaka wa fedha 2024/ 2025
Katika baraza hilo la madiwani likiongozwa na makamu mwenyekiti wa baraza, Mhe Keremba Irobi pamoja na mambo mengine lilipokea na kujadili taarifa ya TARURA, RUWASSA na Taarifa ya mthibiti ubora wa shule halmashauri ya wilaya ya Bunda.
Tuesday, 11 February 2025
Waandishi redio jamii Kanda ya Ziwa wajengewa uwezo kuhusu marburg
11 February 2025,
Dr. Chikondi Khangamwa mtaalam wa jamii na tabia kutoka UNICEF
Dalili za awali za ugonjwa huu hazitofautiani sana na ugonjwa wa maralia kama vile homa kali, maumivu ya kichwa, maumivu ya mgongo, maumivu ya misuli, na kutapika na saa nyingine ngonjwa anaweza kutapika damu.
Na Adelinus Banenwa
Mtandaoni wa Redio za Kijamii Tanzania TADIO kwa kushirikiana na serikali pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya watoto UNICEF wamefungua mafunzo kwa waandishi wa habari wa redio jamii Kanda ya Ziwa yenye lengo la kuwajengea uelewa waandishi hao kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa marburg.
Kaimu afisa afya mkoa wa kagera ndugu Salumu Kimbau
Mafunzo hayo kwa waandishi wa habari yanafanyika mjini Bukoba mkoani Kagera ambapo mlipuko wa ugonjwa huo kwa mara mbili umezuka katika wilaya ya Biharamulo.
Akizungumza katika mafunzo hayo, Kaimu Afisa Afya Mkoa wa Kagera Bw. Salumu Kimbau amesema serikali inatambua sana mchango wa vyombo vya habari na wanahabari katika kupeleka taarifa sahihi kwa jamii kutokana na changamoto mbalimbali za kiafya zinapojitokeza kama vile magonjwa ya milipuko kama ulivyo ugonjwa wa marburg lengo ni kuondoa taharuki kwenye jamii.
Baadhi ya waandishi wa habari wa redio jamii Kanda ya Ziwa katika mafunzo mkoani Kagera
Akizungumzia ugonjwa wa marburg ndugu Kimbau amesema dalili za awali za ugonjwa huu hazitofautiani sana na ugonjwa wa maralia kama vile homa kali, maumivu ya kichwa, maumivu ya mgongo, maumivu ya misuli, na kutapika na saa nyingine ngonjwa anaweza kutapika damu huku hatua mbaya zaidi katika ugonjwa huu ni pale ugonjwa anapoanza kutokwa na damu sehemu za wazi za mwili wake.
Kimbau ameongeza kuwa hadi sasa ugonjwa wa Marburg hauna chanjo wala tiba isipokuwa ngonjwa anatibiwa tu dalili zinazokuwa zinajitokeza kama vile homa, maumivu ya kichwa n.k huku akisisitiza kuwa dalili za ugonjwa huu kujitokeza kati ya siku moja hadi siku 21 ambapo wahisiwa wote huwekwa karantini kwa lengo la kufuatiliwa ikiwa wameathirika na ugonjwa huo la.
Katika hatua nyingine Kimbau amesema ugonjwa huo huenezwa kwa kugusana na muathirika wa ugonjwa huo kupitia majimaji inaweza kuwa ni jssho, mate, kujamiiana, kugusa vyombo au matandiko ya mgonjwa lakini hadi sasa hakuna utafiti unaoonesha kuwa ugonjwa huo unaenezwa kwa njia ya hewa.
Naye Dr. Chikondi Khangamwa Mtaalamu wa jamii na tabia kutoka UNICEF amesema shirika hilo la umoja wa mataifa limeamua kushirikiana na serikali pamoja na TADIO kutokana na sera zao ambapo wanaamini mara nyingi kwenye majanga kama vile magonjwa ya milipuko, vita na majanga ya asili waathirika wakubwa ni watoto hivyo hata katika mlipuko huu wa ugonjwa wa Marburg mkoani Kagera wamelazimika kushiriki kwa kuwa mtoto alipo basi UNICEF wapo.
Monday, 10 February 2025
Bunda: Mwili wa mvuvi aliyezama ziwa Victoria wapatikana
11 February 2025,
Baadhi ya wananchi na wanafamilia wakiwa kando ya ziwa Victoria wakishuhudia zoezi la utafutaji wa aliyezama maji (picha na Yohana)
Aliyepotelea ziwani akiwa kwenye shughuli ya uvuvi, mwili wake umepatikana ikiwa ni siku ya tano tangu alipotoweka.
Na Edward Lucas
Kusekwa Fanuel Rufundya (31) mkazi wa kata ya Guta halmashauri ya mji wa Bunda aliyepotelea ziwani akiwa kwenye shughuli ya uvuvi, mwili wake umepatikana ikiwa ni siku ya tano tangu alipotoweka
Mwili huo umepatikana majira ya alasiri baada ya jitihada za wavuvi na wananchi katika zoezi la utafutaji tangu tarehe 7 Feb 2025 majira ya saa 2:00 asubuhi lilipotokea tukio hilo wakati marehemu na wenzake wawili wakiwa kwenye mtumbwi kwa uvu
Makongo Moni ni mmoja wa wavuvi waliokuwa na marehemu wakati wa tukio, ameiambia redio Mazingira Fm kuwa wakati wakiwa kwenye ‘mashua’ wanaelekea zilipo ndoano zao ndipo upepo ulizidi na mawimbi makali vilitokea jambo lililosababisha chombo chao kujaa maji na kuanza kuzama na katika jitihada za kujiokoa marehemu alishindwa kutokana na kukosa uzoefu wa kuogelea
Makongo Moni ni mmoja wa wavuvi waliokuwa na marehemu
Sunday, 9 February 2025
Bunda: Mvuvi atumbukia ziwa Victoria, siku ya tatu hajapatikana
9 February 2025,
Baadhi ya wananchi na wanafamilia wakiwa kando ya ziwa Victoria wakishuhudia zoezi la utafutaji wa aliyezama maji (Picha na Yohana)
By Edward Lucas
Mtu mmoja Aliyefahamika kwa jina la Kusekwa Fanuel Rufundya (31) mkazi wa mtaa wa Ihale kata ya Guta anahofiwa kufariki dunia kwa kuzama ndani ya maji wakati akiwa katika shughuli za uvuvi ziwa victoria kata ya Guta halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara.
Mwenyekiti wa mtaa wa Guta Mjini, Steven Malweta Mabusi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo Ijumaa tarehe 7 Feb 2025 majira ya saa 02:00 asubuhi wakati mtu huyo akiwa kwenye mashua (mtumbwi) na wenzake wawili wakiendelea na shughuli za uvuvi ndipo ghafla alitoweka na juhudi za wenzake kuanza kumtafuta zilizanza kwa haraka bila ya mafanikio yoyote
Steven Malweta Mabusi, mwenyekiti wa mtaa
Misoji Rufundya ni Mama mkubwa wa Kusekwa Rufundya ambaye yuko katika eneo la tukio ameeleza kwa namna alivyopokea taarifa ya kijana wao kuzama majiniI
Misoji Rufundya
Saturday, 8 February 2025
Mikoa, halmashauri zapewa maelekezo vita dhidi ya ukeketaji
8 February 2025, 10:18 pm
Waziri wa Maendeleo ya jamii jinsia wanawake na makundi maalumu Dr. Doroth Gwajima
Waziri Gwajima ameiagiza mikoa yote inayoongoza kwa ukeketaji nchini kutenga bajeti za kutekeleza afua za kupinga ukeketaji ikiwa ni pamoja na kuwahudumia manusura wa ukatili wa ukeketaji na ukatili mwingine.
Na Adelinus Banenwa
Waziri wa Maendeleo ya jamii jinsia wanawake na makundi maalumu Dr. Doroth Gwajima ameiagiza mikoa yote inayoongoza kwa ukeketaji nchini kutenga bajeti za kutekeleza afua za kupinga ukeketaji ikiwa ni pamoja na kuwahudumia manusura wa ukatili wa ukeketaji na ukatili mwingine ikiwemo kuwawezesha watoa huduma kuwafikia wahanga kwa urahisi.
Dr Gwajima ameyasema hayo leo Feb 8, 2025 wilayani tarime kwenye maadhimisho ya siku ya kupinga ukeketaji Duniani
Waziri Dr Doroth Gwajima na viongozi wengine wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa kituo jumuishi cha huduma kwa wahanga wa matukio ya ukatili Wa kijinsia Nyamwaga Tarime
Maadhimisho hayo ameambatana na uzinduzi wa kituo jumuishi cha huduma kwa wahanga wa matukio ya ukatili eneo la Nyamwaga Tarime kilichogharimu shilingi milioni 186 kwa ufadhili wa shirika la umoja wa mataifa linalojihusisha na idadi ya watu duniani UNFPA ambapo lengo kuu la kituo hicho ni kutoa huduma za pamoja kwa wahanga na manusura wa ukatili ndani ya jengo moja.
Kutuo hicho tangu kilipoanza kufanya kazi mwezi July 2024 hadi sasa manusura wapatao 325 wakiwemo watoto 204 wamehudumiwa ambapo kwa mujibu wa takwimu hizo watoto ndiyo wanaofika kituoni hapo kwa wingi kupata huduma.
Waziri Dr Doroth Gwajima akifungua kibao kuashiria ufunguzi wa kituo jumuishi cha huduma kwa wahanga wa matukio ya ukatili Wa kijinsia Nyamwaga Tarime
Kituo hicho kinatoa huduma za afya, msaada wa kisheria pamoja na ustawi wa jamii lengo likiwa ni kutoa huduma za pamoja kwa manusura wa ukatili ambapo UNFPA kadhalika wamejenga jengo kama hilo katika mkoa wa Shinyanga.
Pia Mhe Gwajima amesema mbinu mpya ya Ukeketaji imeibuka hasa maeneo ya mipakani ambapo makundi ya vijana wa kike huvushwa mipakani na kupelekwa nchi jirani kwa ajiri ya kufanyiwa ukeketaji na kisha kurudishwa nchini bila kubainika pia mangariba vivyo hivyo.
Katika kukabiliana na mbinu hizo mhe Waziri Gwajima ameelekeza vituo vyote jumuishi vikae na kuandaa taarifa yao ya pamoja itayohusisha wataalamu wa afya. Jeshi la polisi na ustawi wa jamii ili muhutasari wao uambatanishwe na MTAKUWA kisha upelekwe ofisi za wilaya kisha mkoani kisha upande kwenda wizarani na wizara zitakaa na kushauri wanasheria kufanya marekebisho ya sheria ya ukeketaji na masuala mengine kama yatakavyokuwa yamependekezwa kutoka kwenye vituo hivyo.
Sauti Waziri wa Maendeleo ya jamii jinsia wanawake na makundi maalumu Dr. Doroth Gwajima
Awali akizungumza katika maadhimisho hayo mkuu wa wilaya ya Bunda Dkt Vicent Naano kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Mara Kanal Evance Mtambi ameiagiza halmashauri ya wilaya ya Tarime kupitia mapato ya ndani kujenga nyumba salama kwa ajili ya watoto wanaofanyiwa ukatili.
Mkuu wa wilaya ya Bunda Dkt Vicent Naano kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Mara
Pia Dr Naano kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Mara ameagiza kutolewa kwa elimu Maafisa wa jeshi la polisi wanaohusika na kuhudumia wahanga wa ukatili ili wawe na mtazamo mmoja katika kushughulikia kesi hizo za ukatili.
Sauti ya mkuu wa wilaya ya Bunda Dkt Vicent Naano
Mark Bryan Schreiner mwakilishi mkazi wa UNFPA nchini Tanzanian amesema tatika kupambana na ukatili wa kijinsia ikiwemo ukeketaji na ndoa za utotoni kunahitajika juhudi za pamoja kati ya wanawake wanaume watoto vijana pamoja na serikali
Mark amesema kupitia program ya chaguo langu haki yangu imeonesha mshikamano na utayari wa serikali katika kutokomeza ukatili huo kwenye jamii.
Michael Marwa kutoka C-SEMA na Valerian Mgani kutoka ATFGM MASANGA taasisi ambazo zimejikita katika kutoa elimu ya ukatili wa kijinsia kwa akinamama na watoto hasa wenye ulemavu GBV wamesema hotuba ya Mhe Waziri wameipokea kwa mikono miwili kutokana kwa kuwa inaonesha namna serikali kwa kushirikiana na wadau wameweza kupunguza kiwango cha ukeketaji nchini na mipango itakayowezesha kuendelea kusaidia kushusha kiwango cha ukeketaji na hata kubaki asilimia 0
Sauti za Michael Marwa kutoka C-SEMA na Valerian Mgani kutoka ATFGM MASANGA