Friday, 14 February 2025

 

Radio Mazingira FM yapongezwa kwa utendaji kazi mzuri

14 February 2025, 

Mkuu wa wilaya ya Musoma Juma Chikoka alipokuwa akizungumzia siku ya radio,(picha na Shomari)

Mkuu huyo wa wilaya ya Musoma amekipongeza kituo cha redio cha Mazingira Fm cha mjini Bunda kwa kazi nzuri za kuendelea kuwafikishia wananchi taarifa mbalimbali.

Na.Shomari Binda

Katika kuadhimisha siku ya radio duniani jamii imetakiwa kufatilia matangazo yake ili kuweza kupata taarifa mbalimbali zikiwemo za utekelezaji wa miradi ya serikali.

Kauli hiyo imetolewa februari 13,2025 na mkuu wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka alipokuwa akiizungumzia siku hiyo.

Amesema redio ni chombo muhimu na kinachopaswa kufatiliwa hivyo wananchi wanakumbushwa kufatilia matangazo yanayotolewa

Chikoko amesema ipo miradi inayotekelezwa na serikali katika Wilaya ya Musoma na maeneo mengine ya nchi na moja ya vyanzo vya kupata taarifa ni kupitia redio

Mkuu huyo wa Wilaya ya Musoma amekipongeza kituo cha redio cha Mazingira Fm cha mjini Bunda kwa kazi nzuri za kuendelea kuwafikishia wananchi taarifa mbalimbali.

Chikoka kupitia siku hii ya redio duniani amewapongeza watangazaji wa Mazingira Fm kwa kazi wanayoifanya ya kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata taarifa

Wednesday, 12 February 2025

 

Wanahabari wapigwa msasa uandishi bila kuleta taharuki

12 February 2025, 

Ili kuwezesha jamii isipate madhara zaidi ni wajibu wa mwandishi wa habari na chombo cha habari kujua namna ya mbinu sahihi za kutumia ili kuleta matokeo chanya ambayo pia hayawezi kuleta taharuki kwenye jamii husika.

Na Adelinus Banenwa

Waandishi wa habari wa redio za kijamii wajengewa uwezo wa namna bora ya kuandika habari na kuandaa vipindi vya afya ambavyo haviwezi kusababisha taharuki kwa jamii ila kutoa elimu na uelewa.

Baadhi ya washiriki wa semina wakiendelea na mafunzo ya mbinu sahihi za uandaaji wa habari

Hayo yamejili leo Feb 11, 2025 ikiwa ni siku ya pili ya semina ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari kutoka redio za kijamii kanda ya ziwa kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa Marburg chini ya Ufadhili wa Shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia masuala ya watoto UNICEF

Prosper Laurent Kwigize mwandishi wa habari na mchambuzi wa masuala ya utatuzi wa migogoro moja kati ya watoa mada amesema ili kuwezesha jamii isipate madhara zaidi ni wajibu wa mwandishi wa habari na chombo cha habari kujua namna ya mbinu sahihi za kutumia ili kuleta matokeo chanya ambayo pia hayawezi kuleta taharuki kwenye jamii husika.

Washiriki wakiendelea kupata uzoefu wa uandaaji wa habari za afya

Ndugu proper amesema kuwa mara nyingi kwenye changamoto za magonjwa hasa ya milipuko yanapotokea watu wanataka kujua je vyombo vya habari vinasema nini hivyo ni wajibu wa chombo cha habari au mwanahabari mwenyewe kuseti ajenda ambayo kupitia maswali yake yanaweza kusaidia kutoa mwelekeo kwa jamii kuhusu ugonjwa husika.

 

Bunda: Shule kukosa mwalimu wa kike, DC atoa maagizo mazito

12 February 2025, 

Dr Vicent Naano Anney, DC Bunda akizungumza katika baraza la madiwani halmashauri ya wilaya (Picha na Edward Lucas)

Kati ya walimu 350 waliopo halmashauri ya wilaya ya Bunda walimu wa kike ni 45 pekee.

Na Edward Lucas

Kutokana na kilio cha kukosa mwalimu wa kike shule ya sekondari Tirina, mkuu wa wilaya ya Bunda, Dr Vicent Naano Anney amempa siku moja mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo awe amempa barua ya kuonesha mwalimu amepelekwa katika shule hiyo

Naano ametoa maagizo hayo leo kupitia mkutano wa baraza la madiwani kupokea taarifa mbalimbali ya robo ya pili ya mwaka wa fedha 2024/2025 katika halmashauri ya wilaya ya Bunda

George Stanley Mbilinyi, DED halmashauri ya wilaya ya Bunda akiwa katika mkutano wa Baraza la Madiwani (Picha na Edward Lucas)

Awali akizungumzia changamoto hiyo diwani wa kata ya Mugeta, Mganga Jongora amesema shule ya sekondari Tirina ina wanafunzi wa kike na wa kiume lakini toka shule hiyo ifunguliwe haina mwalimu wa kike jambo linalosababisha wanafunzi wa kike wakose mtu wa kumfikishie changamoto zao

Sauti ya Mganga Jongora, Diwani wa Mugeta

Katika mahojiano na Mazingira Fm, Kaimu Afisa Elimu Sekondari wa halmashauri ya wilaya ya Bunda, Nambua Godfrey Semlugu amekiri kuwepo changamoto ya uhaba wa walimu wa kike kwani kati ya walimu 350 wa kike ni 45 pekee.

Sauti ya Nambua G. Semlugu

 

Dkt. Naano: Safari hii kwenye bajeti Bunda DC lipeni madeni ya watu

13 February 2025, 

Dr Vicent Naano Anney, DC Bunda akizungumza katika baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya Bunda (Picha na Edward Lucas)

Halmashauri ya wilaya ya Bunda yatakiwa mwaka huu kwenye bajeti kutenge fedha kwa ajili ya kulipa madeni ya wadau mbalimbali.

By Edward Lucas.

Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Dr Vicent Naano Anney amemwagiza mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Bunda mwaka huu kwenye bajeti watenge fedha kwa ajili ya kulipa madeni ya wadau mbalimbali

Amesema ni aibu kuona watu wanajitokeza mara kwa mara wakidai pesa zao katika halmashauri ambazo waliingia nazo mikataba na kutoa tahadhari kwa miradi mipya inayotekelezwa awamu hii kuingia katika madeni

Sauti ya Dr.Vicent Naano, DC Bunda

Naano ameyasema hayo katika mkutano wa baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya Bunda lililofanyika jana tarehe 12 Feb 2025 kupokea taarifa ya robo ya pili ya mwaka wa fedha 2024/ 2025

Katika baraza hilo la madiwani likiongozwa na makamu mwenyekiti wa baraza, Mhe Keremba Irobi pamoja na mambo mengine lilipokea na kujadili taarifa ya TARURA, RUWASSA na Taarifa ya mthibiti ubora wa shule halmashauri ya wilaya ya Bunda.

Tuesday, 11 February 2025

 

Waandishi redio jamii Kanda ya Ziwa wajengewa uwezo kuhusu marburg

11 February 2025, 

Dr. Chikondi Khangamwa mtaalam wa jamii na tabia kutoka UNICEF

Dalili za awali za ugonjwa huu hazitofautiani sana na ugonjwa wa maralia kama vile homa kali, maumivu ya kichwa, maumivu ya mgongo, maumivu ya misuli, na kutapika na saa nyingine ngonjwa anaweza kutapika damu.

Na Adelinus Banenwa

Mtandaoni wa Redio za Kijamii Tanzania TADIO kwa kushirikiana na serikali pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya watoto UNICEF wamefungua mafunzo kwa waandishi wa habari wa redio jamii Kanda ya Ziwa yenye lengo la kuwajengea uelewa waandishi hao kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa marburg.

Kaimu afisa afya mkoa wa kagera ndugu Salumu Kimbau

Mafunzo hayo kwa waandishi wa habari yanafanyika mjini Bukoba mkoani Kagera ambapo mlipuko wa ugonjwa huo kwa mara mbili umezuka katika wilaya ya Biharamulo.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Kaimu Afisa Afya Mkoa wa Kagera Bw. Salumu Kimbau amesema serikali inatambua sana mchango wa vyombo vya habari na wanahabari katika kupeleka taarifa sahihi kwa jamii kutokana na changamoto mbalimbali za kiafya zinapojitokeza kama vile magonjwa ya milipuko kama ulivyo ugonjwa wa marburg lengo ni kuondoa taharuki kwenye jamii.

Baadhi ya waandishi wa habari wa redio jamii Kanda ya Ziwa katika mafunzo mkoani Kagera

Akizungumzia ugonjwa wa marburg ndugu Kimbau amesema dalili za awali za ugonjwa huu hazitofautiani sana na ugonjwa wa maralia kama vile homa kali, maumivu ya kichwa, maumivu ya mgongo, maumivu ya misuli, na kutapika na saa nyingine ngonjwa anaweza kutapika damu huku hatua mbaya zaidi katika ugonjwa huu ni pale ugonjwa anapoanza kutokwa na damu sehemu za wazi za mwili wake.

Kimbau ameongeza kuwa hadi sasa ugonjwa wa Marburg hauna chanjo wala tiba isipokuwa ngonjwa anatibiwa tu dalili zinazokuwa zinajitokeza kama vile homa, maumivu ya kichwa n.k huku akisisitiza kuwa dalili za ugonjwa huu kujitokeza kati ya siku moja hadi siku 21 ambapo wahisiwa wote huwekwa karantini kwa lengo la kufuatiliwa ikiwa wameathirika na ugonjwa huo la.

Katika hatua nyingine Kimbau amesema ugonjwa huo huenezwa kwa kugusana na muathirika wa ugonjwa huo kupitia majimaji inaweza kuwa ni jssho, mate, kujamiiana, kugusa vyombo au matandiko ya mgonjwa lakini hadi sasa hakuna utafiti unaoonesha kuwa ugonjwa huo unaenezwa kwa njia ya hewa.

Naye Dr. Chikondi Khangamwa Mtaalamu wa jamii na tabia kutoka UNICEF amesema shirika hilo la umoja wa mataifa limeamua kushirikiana na serikali pamoja na TADIO kutokana na sera zao ambapo wanaamini mara nyingi kwenye majanga kama vile magonjwa ya milipuko, vita na majanga ya asili waathirika wakubwa ni watoto hivyo hata katika mlipuko huu wa ugonjwa wa Marburg mkoani Kagera wamelazimika kushiriki kwa kuwa mtoto alipo basi UNICEF wapo.

Monday, 10 February 2025

 

Bunda: Mwili wa mvuvi aliyezama ziwa Victoria wapatikana

11 February 2025, 

Baadhi ya wananchi na wanafamilia wakiwa kando ya ziwa Victoria wakishuhudia zoezi la utafutaji wa aliyezama maji (picha na Yohana)

Aliyepotelea ziwani akiwa kwenye shughuli ya uvuvi, mwili wake umepatikana ikiwa ni siku ya tano tangu alipotoweka.

Na Edward Lucas

Kusekwa Fanuel Rufundya (31) mkazi wa kata ya Guta halmashauri ya mji wa Bunda aliyepotelea ziwani akiwa kwenye shughuli ya uvuvi, mwili wake umepatikana ikiwa ni siku ya tano tangu alipotoweka

Mwili huo umepatikana majira ya alasiri baada ya jitihada za wavuvi na wananchi katika zoezi la utafutaji tangu tarehe 7 Feb 2025 majira ya saa 2:00 asubuhi lilipotokea tukio hilo wakati marehemu na wenzake wawili wakiwa kwenye mtumbwi kwa uvu

Makongo Moni ni mmoja wa wavuvi waliokuwa na marehemu wakati wa tukio, ameiambia redio Mazingira Fm kuwa wakati wakiwa kwenye ‘mashua’ wanaelekea zilipo ndoano zao ndipo upepo ulizidi na mawimbi makali vilitokea jambo lililosababisha chombo chao kujaa maji na kuanza kuzama na katika jitihada za kujiokoa marehemu alishindwa kutokana na kukosa uzoefu wa kuogelea

Makongo Moni ni mmoja wa wavuvi waliokuwa na marehemu

Sunday, 9 February 2025

 

Bunda: Mvuvi atumbukia ziwa Victoria, siku ya tatu hajapatikana

9 February 2025, 

Baadhi ya wananchi na wanafamilia wakiwa kando ya ziwa Victoria wakishuhudia zoezi la utafutaji wa aliyezama maji (Picha na Yohana)

By Edward Lucas

Mtu mmoja Aliyefahamika kwa jina la Kusekwa Fanuel Rufundya (31) mkazi wa mtaa wa Ihale kata ya Guta anahofiwa kufariki dunia kwa kuzama ndani ya maji wakati akiwa katika shughuli za uvuvi ziwa victoria kata ya Guta halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara.

Mwenyekiti wa mtaa wa Guta Mjini, Steven Malweta Mabusi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo Ijumaa tarehe 7 Feb 2025 majira ya saa 02:00 asubuhi wakati mtu huyo akiwa kwenye mashua (mtumbwi) na wenzake wawili wakiendelea na shughuli za uvuvi ndipo ghafla alitoweka na juhudi za wenzake kuanza kumtafuta zilizanza kwa haraka bila ya mafanikio yoyote

Steven Malweta Mabusi, mwenyekiti wa mtaa

Misoji Rufundya ni Mama mkubwa wa Kusekwa Rufundya ambaye yuko katika eneo la tukio ameeleza kwa namna alivyopokea taarifa ya kijana wao kuzama majiniI

Misoji Rufundya

Saturday, 8 February 2025

 

Mikoa, halmashauri zapewa maelekezo vita dhidi ya ukeketaji

8 February 2025, 10:18 pm

Waziri wa Maendeleo ya jamii jinsia wanawake na makundi maalumu Dr. Doroth  Gwajima

Waziri Gwajima ameiagiza mikoa yote inayoongoza kwa ukeketaji nchini kutenga bajeti za kutekeleza afua za kupinga ukeketaji ikiwa ni pamoja na kuwahudumia manusura wa ukatili wa ukeketaji na ukatili mwingine.

Na Adelinus Banenwa

Waziri wa Maendeleo ya jamii jinsia wanawake na makundi maalumu Dr. Doroth  Gwajima ameiagiza mikoa yote inayoongoza kwa ukeketaji nchini kutenga bajeti za kutekeleza afua za kupinga ukeketaji ikiwa ni pamoja na kuwahudumia manusura wa ukatili wa ukeketaji na ukatili mwingine ikiwemo kuwawezesha watoa huduma kuwafikia wahanga kwa urahisi.

Dr Gwajima ameyasema hayo leo Feb 8, 2025 wilayani tarime kwenye maadhimisho ya siku ya kupinga ukeketaji Duniani

Waziri Dr Doroth Gwajima na viongozi wengine wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa kituo jumuishi cha huduma kwa wahanga wa matukio ya ukatili Wa kijinsia Nyamwaga Tarime

Maadhimisho hayo ameambatana na uzinduzi wa kituo jumuishi cha huduma kwa wahanga wa matukio ya ukatili eneo la Nyamwaga Tarime kilichogharimu shilingi milioni 186 kwa ufadhili wa shirika la umoja wa mataifa linalojihusisha na idadi ya watu duniani UNFPA ambapo lengo kuu la kituo hicho ni kutoa huduma za pamoja kwa wahanga na manusura wa ukatili ndani ya jengo moja.

Kutuo hicho tangu kilipoanza kufanya kazi mwezi July 2024 hadi sasa manusura wapatao 325 wakiwemo watoto 204 wamehudumiwa ambapo kwa mujibu wa takwimu hizo watoto ndiyo wanaofika kituoni hapo kwa wingi kupata huduma.

Waziri Dr Doroth Gwajima akifungua kibao kuashiria ufunguzi wa kituo jumuishi cha huduma kwa wahanga wa matukio ya ukatili Wa kijinsia Nyamwaga Tarime

Kituo hicho kinatoa huduma za afya,  msaada wa kisheria pamoja na ustawi wa jamii lengo likiwa ni kutoa huduma za pamoja kwa manusura wa ukatili ambapo UNFPA kadhalika wamejenga jengo kama hilo katika mkoa wa Shinyanga.

Pia Mhe Gwajima amesema mbinu mpya ya Ukeketaji imeibuka hasa maeneo ya mipakani ambapo makundi ya vijana wa kike huvushwa mipakani na kupelekwa nchi jirani kwa ajiri ya kufanyiwa ukeketaji na kisha kurudishwa nchini bila kubainika pia mangariba vivyo hivyo.

Katika kukabiliana na mbinu hizo mhe Waziri Gwajima ameelekeza vituo vyote jumuishi vikae na kuandaa taarifa yao ya pamoja itayohusisha wataalamu wa afya. Jeshi la polisi na ustawi wa jamii ili muhutasari wao uambatanishwe na MTAKUWA kisha upelekwe ofisi za wilaya kisha mkoani kisha upande kwenda wizarani na wizara zitakaa na kushauri wanasheria kufanya marekebisho ya sheria ya ukeketaji na masuala mengine kama yatakavyokuwa yamependekezwa kutoka kwenye vituo hivyo.

Sauti Waziri wa Maendeleo ya jamii jinsia wanawake na makundi maalumu Dr. Doroth  Gwajima

Awali akizungumza katika maadhimisho hayo mkuu wa wilaya ya Bunda Dkt Vicent Naano kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Mara Kanal Evance Mtambi  ameiagiza halmashauri ya wilaya ya Tarime kupitia mapato ya ndani kujenga nyumba salama kwa ajili ya watoto wanaofanyiwa ukatili.

Mkuu wa wilaya ya Bunda Dkt Vicent Naano kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Mara

Pia Dr Naano kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Mara ameagiza kutolewa kwa elimu Maafisa wa jeshi la polisi wanaohusika na kuhudumia wahanga wa ukatili ili wawe na mtazamo mmoja katika kushughulikia kesi hizo za ukatili.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Bunda Dkt Vicent Naano

Mark Bryan Schreiner mwakilishi mkazi wa UNFPA nchini Tanzanian amesema tatika kupambana na ukatili wa kijinsia ikiwemo ukeketaji na ndoa za utotoni kunahitajika juhudi za pamoja kati ya wanawake wanaume watoto vijana pamoja na serikali

Mark amesema kupitia program ya chaguo langu haki yangu imeonesha mshikamano na utayari wa serikali katika kutokomeza ukatili huo kwenye jamii.

Michael Marwa kutoka C-SEMA na Valerian Mgani kutoka ATFGM MASANGA taasisi ambazo zimejikita katika kutoa elimu ya ukatili wa kijinsia kwa akinamama na watoto hasa wenye ulemavu GBV wamesema hotuba ya Mhe Waziri wameipokea kwa mikono miwili kutokana kwa kuwa inaonesha namna serikali kwa kushirikiana na wadau wameweza kupunguza kiwango cha ukeketaji nchini na mipango itakayowezesha kuendelea kusaidia kushusha kiwango cha ukeketaji na hata kubaki asilimia 0

Sauti za Michael Marwa kutoka C-SEMA na Valerian Mgani kutoka ATFGM MASANGA

Thursday, 6 February 2025

 

Kamati ya fedha Bunda TC yakagua miradi, yaipa tano Bunda Mjini Sec

6 February 2025, 

Nyumba ya walimu Bunda mjini Sekondari ambayo itagharimu milion 100 hadi kukamilika kwake

Wananchi watakiwa kulinda miradi ili iweze kudumu na kuhudumia kizazi cha sasa na hata kile kijacho

Na Adelinus Banenwa

Kiasi cha shilingi milioni 88 kimeshatumika kati ya shilingi milioni 100 kwenye ujenzi wa Nyumba ya walimu shule ya sekondari Bunda mjini mkoani Mara

Mkuu wa shule ya sekondari ya Bunda mjini amesema nyumba hiyo imejengwa katika mfumo wa Nyumba mbili ndani ya moja ambayo familia mbili za walimu wataishi pindi itakapokamilika.

Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Bunda na diwani wa kata ya Sazira Mhe Michael Kweka, Akisaini kitabu cha wageni baada ya ukaguzi

Ufafanuzi huu umetolewa kwa kamati ya fedha ya halmashauri ya mji wa Bunda iliyofika shuleni hapo kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo wa nyumba ya mwalimu.

Katika ujumbe wake mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Bunda na diwani wa kata ya Sazira Mhe Michael Kweka mbali na kupongeza mkuu wa shule kwa usimamizi mzuri wa mradi amemtaka kukamilisha ujenzi huo kwa wakati ili nyumba hiyo iweze kutumika.

Sauti ya mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Bunda na diwani wa kata ya Sazira Mhe Michael Kweka

Kwa upande wake mkurugenzi wa mji wa Bunda Juma Haji ametoa wito kwa wananchi kuhakikisha wailinda miundombinu inayoletwa na serikali katika maeneo yao ili iendelee kuhudumia kizazi cha sasa na hata kijacho.

Sauti ya mkurugenzi wa mji wa Bunda Juma Haji

Monday, 3 February 2025

 

Zaidi ya watu 2700 wafikiwa wiki ya sheria Bunda

3 February 2025, 

Mulokozi Kamuntu hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Bunda, katika kilele wiki ya sheria

Wananchi zaidi ya 2700 wamefikiwa wiki ya sheria wilayani Bunda baada ya kufika katika vituo vilivyokuwa vimeainishwa na wadau wa mahakama.

Na Adelinus Banenwa

Wananchi zaidi ya 2700 wamefikiwa wiki ya sheria wilayani Bunda baada ya kufika katika vituo vilivyokuwa vimeainishwa na wadau wa mahakama.

Hayo yamesemwa na Mulokozi Kamuntu hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Bunda katika kilele cha maadhimisho wiki ya sheria ambapo kwa wilaya ya Bunda maadhimisho hayo yakifanyika leo Feb 3, 2025 kwenye viwanja vya mahakama ya wilaya ya Bunda.

Sauti ya Mulokozi Kamuntu hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Bunda
Mkuu wa wilaya ya Bunda Dkt Vicent Naano katika kilele wiki ya sheria

Katika maadhimisho hayo mkuu wa wilaya ya Bunda Dkt Vicent Naano akiwa mgeni wa heshima ameipongeza mahakama wilayani Bunda kwa kufuata sheria katika kutekeleza majikumu yake hali ambayo amedai inapunguza tabia ya mahakama kulalamikiwa katika utendaji wa haki.

Baadhi aya watumishi wa mahakama wilayani Bunda katika kilele wiki ya sheria

Pia amewashukuru wadau wote wa sheria ikiwemo ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali, ofisi ya mawakili chini ya TLS huku akiwanyooshea vidole baadhi ya mawakili wasiyokuwa waaminifu katika utendaji wao wa kazi .

Sauti Mkuu wa wilaya ya Bunda Dkt Vicent Naano