Ni katika Mahafali ya Kidato cha 4 shule ya Sekondari Kabasa, Kambarage Wasira akiwa mgeni rasmi atoa milioni 1 (1,000,000/=Tsh) kukabili sehemu ya changamoto katika shule hiyo.
Wahitimu wa kidato cha 4 Sekondari Kabasa wakifanya yao mbele ya wageni waalikwa.Shangwe kama lote kwa walimu na wanafunzi Kabasa SekondariMiongoni mwa wageni waalikwa ilikuwa ni pamoja na walimu kutoka shule mbalimbali wilaya ya BundaKambarage Wasira akizungumza katika mahafali ya 17 shule ya Sekondari Kabasa. Picha na Edward Lucas
Na Edward Lucas
Ikiwa ni wiki moja imepita tangu Kambarage ashiriki mahafali ya darasa la saba shule ya msingi Kunzugu na kutoa ahadi ya ‘Printa’ yenye thamani ya milioni 1 na laki 2 (1,200,000/=) hii leo ilikuwa ni zama ya Sekondari Kabasa akiwa mgeni rasmi tena.
Katika mahafali hayo, Kambarage Wasira ametoa shilingi milioni 1 ili kusaidia sehemu ya changamoto zinazoikabiri shule hiyo.
Sauti ya Kambarage WasiraGodfrey Maige Maduhu, Mkuu wa shule ya Sekondari Kabasa. Picha na Edward Lucas
Awali akisoma taarifa ya shule, Mkuu wa shule hiyo, Godfrey Maige Maduhu amebainisha changamoto mbalimbali zinazoikabiri shule hiyo kuwa ni pamoja na ukosefu wa bwalo, maktaba, upungufu wa walimu na upungufu wa matundu ya choo 24 huku akiipongeza serikali ya awamu ya sita kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa kwani shule hiyo ina madarasa ya ziada 6
Sauti ya Godfrey Maige MaduhuGrace Raymond akisoma risala ya wahitimu kidato cha 4 Sekondari Kabasa ikibainisha baadhi ya changamoto walizokumbana nazoSauti ya Grace Raymond
Baadhi ya viongozi wa NMB na serikali wakipeana mikono baada ya kukabidhi Madawati, Picha na Adelinus Banenwa
Katika kuadhimisha wiki ya wateja banke ya NMB tawi la bunda wametoa msaada wa madawati 100 kwa sule ya msingi ya nyasura iliyopo kata ya nyasura halamshauri ya mji wa bunda mkoani mara.
Na Adelinus Banenwa
Katika kuadhimisha wiki ya wateja banke ya NMB tawi la bunda wametoa msaada wa madawati 100 kwa sule ya msingi ya nyasura iliyopo kata ya nyasura halamshauri ya mji wa bunda mkoani mara.
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi madawati hayo mkuu wa taasisi za serikali na taasisi binafsi banki ya NMB William Makoresho amesema banki hiyo imekuwa ikishiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii kama vile sekta ya elimu, afya na uelimishaji wa mambo mbalimbali.
Amesema katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa mteja wamewiwa kutoa msaada huo kwa shule ya Nyasura kutokana na mahitaji yake ambapo dawati 100 zilizotolewa zimegharimu shilingi 12 milioni.
Mkuu wa taasisi za serikali na taasisi binafsi banki ya NMB William Makoresho, Picha na Adelinus BanenwaSauti ya mkuu wa taasisi za serikali na taasisi binafsi banki ya NMB William Makoresho
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Bunda Dr Vicent Anney Naano ameishukuru bank ya NMB kwa kutoa msaada huo huku akibainisha kwa wilaya ya Bunda inaupungufu wa madawati elfu 16 huku halmashauri ya mji wa Bunda ikiwa na upungufu wa madawati elfu 6 .
Mkuu wa wilaya ya Bunda Dr Vicent Anney Naano, Picha na Adelinus BanenwaSauti ya mkuu wa wilaya ya Bunda Dr Vicent Anney Naano,
Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule ya msingi Nyasura mwalimu Benard Ngero Paul amesema ujio wa madawati hayo kama msaada kutoka NMB utapunguza changamoto ya uhaba wa madawati japo bado yanaitajika madawati mengi kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi walioko shuleni hapo.
Mwalimu Benard amesema shule ya nyasura ina wanafunzi wapatao 1775 ambapo wasichana ni 985 na wavilana ni 790 ambao wanaitaji madawati 591 huku yaliyopo ni 197 huku upungufu ukitajwa ni madawati 394.
Aidha amebainisha changamoto nyingine ni matundu ya vyoo ambapo kwa mahitaji ni matundu 60 ya vyoo ila yaliyopo ni 12 tu.
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Nyasura mwalimu Benard Ngero Paul